Searching...
Jumatatu, 13 Januari 2014

SIRI NZITO JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI-KENYA,UGANDA NA RWANDA WAKUBALIANA HIMAYA MOJA YA ULINZI,RUKSA KUINGILIA VITA MOJA INAPOVAMIWA.

MARAIS WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI-KUTOKA KUSHOTO: UHURU KENYATTA, YOWERI MUSEVENI NA PAUL KAGAME.

Mawaziri wa ulinzi na wa mambo ya ndani kutoka nchi za Uganda,Rwanda na Kenya wametia saini makubaliano kuweka himaya moja ya ulinzi miongoni mwa nchi hizo. Hii ni mara ya kwanza kuwepo kwa mkataba huo na hii ina maana nchi moja ikipata matatizo ya usalama nchi nyingine zitakuwa na uhuru wa kuingilia kati na kusaidia. Kikao cha mawaziri hao kilitanguliwa na kile cha wakuu wa majeshi na polisi kutoka nchi hizo ambacho pia kilitathmini changamoto za kiusalama kwenye eneo hilo na jinsi ya kuimarisha ushirikiano miongoni mwa mataifa hayo. Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi. Kusikiliza ripoti hiyo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mwandishi: 
Sylivanus Karemera-BBC

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!