MarehemuEusebio Da Silva Ferreira enzi za uhai wake akikipiga na klabu ya Benfika ya ureno.
Christian Ronaldo akipokea tuzo ya kiatu cha dhahabu mwaka 2011kutoka kwa Eusebio
Enzi za uhai wake marehemu Eusebio akifurahia jambo na Michel Platin pamoja naye Johan Cruyf katika moja ya fainali za Uefa.
Eusebio da Silva Ferreira,ni mmoja kati ya wachezaji maarufu na wa aina yake waliowahi kuitikisa dunia katika tasnia ya soma miaka ya 60 na ni raia wa Ureno ambapo aliwahi kuichezea timu ya Benfica na kuiwezesha timu hiyo kutinga fainali za Uropa.
Eusebio da Silva Ferreira pia alifahamika kwa jina la utania la ‘The Black Pearl’ au
‘Black Panther’
Eusebio aliwahi kutwaa tuzo ya kiatu cha dhahabu kama mfungaji bora wa kombe la dunia mwaka 1966 ambapo aliifungia Ureno magoli nane,yakiwa ni magoli matatu zaidi ya aliyekua ameshikilia rekodi hiyo kipindi hicho.
Eusebio pia aliwahi kuwa mchezaji bora wa mwaka barani ulaya mwaka 1965 na mchezaji bora wa BBC mwaka 1966
Aliwahi kushinda vikombe 64 na kufunga magoli 41.
Eusebio amefunga magoli 441 katika historia yake ya soka baada ya kushuka dimbani mara 447 katika kipindi cha miaka 20 ya historia ya maisha yake katika soka.
Eusebio alimalizia historia ya soka lake kunako klabu ya New Jersey ya Marekani katika ligi ya American Soccer League.
Eusebio alizaliwa Nchini Msumbiji , Eusebio alikua mwaafrika wa kwanza kufanya mabo makubwa katika historia ya soka duniani.
0 comments:
Chapisha Maoni