HALI SIO SHWARI AFRIKA YA KATI,UFARANSA YAINGILIA KATI
Home
»
Unlabelled
» HALI SIO SHWARI AFRIKA YA KATI,UFARANSA YAINGILIA KATI
MAJESHI YA UFARANSA YAKIPIGA DORIA JIJINI BANGUI Hali katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika
kati-Bangui,bado inatisha baada ya mapigano ya umwagaji damu kati ya makundi ya imani
tofauti za kidini.Hata hivyo jeshi la Ufaransa linasema hali bado
inatisha. Waziri wa ulinzi wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian amesema mpango wa
kuwapokonya silaha wafuasi wa makundi tofauti ya wanamgambo unaanza hii
leo.Ameonya jeshi la Ufaransa linaweza kutumia nguvu kuwalazimisha
wanamgambo wazisalimishe silaha zao.Katika mahojiano na kituo cha
matangazo cha RTL waziri huyo wa ulinzi wa Ufaransa amesema baadhi ya
makundi ya wanamgambo wameanza kuchanganyika na raia wa kawaida na
kusababisha "vurugu". WAZIRI MKUU WA JAMUHURI YA AFRIKA YA KATI NICOLAS TIANGAYE. Wakaazi wa mji mkuu Bangui wamezungumzia kuhusu milio ya hapa na pale ya risasi katika baadhi ya mitaa ya mji huo.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa shirika la haki za binaadamu la Jamhuri ya
Afrika kati,Joseph Bindoumi,wanamgambo wa Seleka ambao wengi wao ni
waislam,bado wangalipo mjini Bangui.
"Hali ni tulivu lakini inatisha" amesema msemaji wa jeshi la Ufaransa
kanali Gilles Jaron akiwa mjini Paris.Ufaransa imeamua kutuma jumla ya
wanajeshi 1600 katika Jamhuri ya Afrika kati,1200 kati yao mjini Bangui.
0 comments:
Chapisha Maoni