Flora Mvungi (Hadija) akijifungua.
Kutoka
kwa vyanzo vyake, mbali na picha za mtoto, Mwandishi wetu alilibamba
tukio la Flora akijifungua Jumatano iliyopita katika Hospitali
ya Marie Stopes iliyopo Sinza, Dar.
Flora akiwa hospitali na mumewe H. Baba.
Kwa mujibu wa H. Baba, alifurahishwa kuitwa baba kwani ni kitu
ambacho alikuwa anatamani kwa muda mrefu na Mungu amemtimizia hivyo
anamshukuru kwani ni zawadi kubwa katika maisha yake.
Mtoto wa Flora Mvungi.
Kwa upande wa Flora alikuwa na haya ya kusema: “Namshukuru sana Mungu
kwa sababu niko salama na mwanangu, ukweli mwacheni mama aitwe mama
kwani kuzaa siyo kazi rahisi”.
H. Baba alimalizia kwa kusema kuwa kama walivyosema awali kabla mtoto huyo hajazaliwa kuwa jina lake ataitwa Tanzanite, ndiyo hivyo itakavyokuwa jina hilo ndilo litakalotumika.
H. Baba alimalizia kwa kusema kuwa kama walivyosema awali kabla mtoto huyo hajazaliwa kuwa jina lake ataitwa Tanzanite, ndiyo hivyo itakavyokuwa jina hilo ndilo litakalotumika.



0 comments:
Chapisha Maoni