GARETH BALE
Hatimaye ule usemi usemao chelewa chelewa
utamkuta mwana sio wako yamedhihirika baada ya jana ijumaa usiku klabu
ya Real Madrid kuamua kuichana timu ya Tottenham kwa kusisitiza kwamba
mchezaji wao sio bora sana na wala hana thamani ya paundi milioni 100
wanazozitaka
Mapema wiki hii Bale akiendesha gari lake kati kati ya jiji la London akisubiri kutua Madrid kabla ya jana usiku dili kuharibika.
Uhamisho wa Bale ulitarajiwa kukamilika leo kwa mkataba wa Madrid kulipa fedha hizo kwa mkupuo mmoja.Kwa uamuzi huo sasa Madrid sio tu kwamba watakuwa wameokoa kiasi kikubwa cha fedha zao lakini pia watakua wamemuhakikishia Ronaldo kwamba yeye ndio mchezaji bora na ghali hadi sasa katika rekodi ya soka duniani na kumfanya kuwa na amani na kuendelea kukipiga kunako Bernabeu.
CHRISTIAN RONALDO-MCHEZAJI GHALI DUNIANI.
Real Madrid wamesema kwamba wao wapo tayari kumnunua Bale kwa paundi milioni 78 tu
Milioni mbili nyuma ya Paundi milioni 80 walizomnunulia nazo Christian
Ronaldo akitokea Manchester United ili kuiacha rekodi ya nguli wao mreno kuwa juu kwani Bale hana
thamani ya kumzidi Ronaldo
DANIEL LEVY-MWENYEKITI WA TOTTENHAM
BAADA YA BALE KUWAAMBIA TOTTENHAM KWAMBA ANATAKA KUONDOKA TOTTENHAMA HADI JANA IJUMAA WALIWANUNUA WACHEZAJI WATATU JUU NI ERIKSEN,CHINI KUSHOTO NI CHIRICHES NA CHINI KULIA NI LAMELA.
0 comments:
Chapisha Maoni