Searching...
Jumatano, 17 Julai 2013

KAMATI MBALI MBALI ZA BUNGE ZATEMBELEA TAHA


       Bi. Jacqueline Mkindi mkurugenzi mkuu wa TAHA akiwakaribisha Mh. Rajab Mbarouk Mohammed na Mh. Murtaza Ally Mangungu walipowasili katika ofisi za Tanzania Horticultural Association (TAHA) kwa ajili ya kupata maelezo ya awali kuhusu hali halisi ya maendeleo ya Horticulture nchini Tanzania.
       Bi. Jacqueline Mkindi akiwasilisha maelezo ya awali kuhusu maaendeleo ya Horticulture nchini Tanzania kabla ya wabunge kwenda kutembelea baadhi ya mashamba ya horticulture yanayoendeshwa na kumilikiwa na wakulima wanachama wa TAHA.
Wabunge wakiangalia kitalu cha shamba la Arusha Blooms kilichopandwa maharage machanga ambayo huzalishwa na kuuzwa katika masoko makubwa yaliyo ndani na nje ya nchi, maharage hayo hutumika katika chakula kama mboga.
1.          Moja ya vitalu vya maharage machanga kwenye shamba la Arusha Blooms
         Msimamizi wa kitalu cha maharage machanga, Masawe akitoa maelezo ya teknolojia inayotumika katika kuzalisha mazao ya horticulture shambani hapo.
Wabunge wakiangalia Jembe la kulimia linalokokotwa na trekta ambalo limebuniwa na kutengenezwa kwa gharama nafuu hapa hapa nchini Tanzania.
         Mh. Mahamoud Hassan Mgimwa akiangalia namna ambavyo maharage machanga yamehifadhiwa kwenye pakiti maalumu ambayo hutumika kusafirishia bidhaa ya mazao hayo katika masoko makubwa nje ya nchi.
Mkurugenzi wa Mashamba ya Rijk Zwaan Afrisem Ltd, Heikki Niskala akifafanua jambo kwa wabunge wakati timu  ujumbe wa wabunge ulipofika katika ofisi za mashamba hayo kama sehemu ya ziara yao ya kilimo Mkoani Arusha.
      Awali, Wabunge walipokewa na Wajumbe wa bodi na baadhi ya wafanyakazi kutoka Sekretarieti ya TAHA ambapo walikaribisha na kushiriki kwa pamoja katika chakula cha jioni.
Sehemu ya matunda yaliyopendezesha chakula cha jioni siku hiyo.
Wakurugenzi kutoka bodi ya TAHA, kulia ni ndugu Juma Lossini akisalimiana na Bi. Fatma Riyami
Timu ya TAHA ikiteta jambo na Mh. Jitu Vrajlal Soni (hayupo pichani)
Mh. Mahamoud Hassan Mgimwa akimsikiliza Mkurugenzi wa TAHA kwa umakini wakati wa chakula cha jioni ndani ya hotel ya Mount Meru Arusha.
Wabunge kutoka kamati mbalimbali za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wafanyakazi kutoka Wizara ya Kilimo, Chakula na ushirika wamefanya ziara ya kilimo ambayo pia iliwafikisha kwa wakulima na wanachama wa taasisi ya Tanzania Horticultural Association (TAHA), TAHA ni taasisi kilele inayoundwa na wanachama wakulima wa kilimo cha mazao ya horticulture nchini Tanzania.
Katika ziara hiyo wabunge walipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wajumbe wa bodi na secretariat ya TAHA ambayo iliainisha changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo wakulima wanachama wa  TAHA katika shughuli zao za kila siku. Tazama taswira ya ziara ya wabunge hapa.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!