Searching...
Jumatano, 1 Mei 2013

MOURINHO AFUNGUKA ASEMA ANAONDOKA MADRID ANAENDA ENGLAND



 
KOCHA JOSE MOURINHO.
Kocha wa timu ya Real Madrid Jose Mourinho amesema hatoendelea na kazi yake kama kocha wa Madrid msimu ujao na badala yake amesema na badala yake amesema atakwenda mahali ambapo watu wanataka awepo.

Baada ya mechi ya jumanne aliyoshinda mabao mawili kwa sufuri dhidi ya borusia Dotmund  japo hayakutosha kuwapeleka fainali Morinyo alisema

 "Najua napendwa sana England, Najua napendwa na vilabu kadhaa pale England na zaidi ni klabu moja maalum"

Lakini akasisitiza kwamba atasubiri kuchukua maamuzi hadi hapo msimu utakapomalizika"sijachukua maamuzi yoyote kuhusu maisha yangu baada ya hapa mpaka sahivi kwasababu bado nina mkataba na klabu na ninauheshimu mkataba wangu na na klabu pamoja na rais wa klabu,nataka kukaa chini na rais nizungumze naye kuhusu uamuzi huu.

 Mourinho aliiacha klabu ya Chelsea the Blues katika hali tete mwezi September 2007, baada ya kushindwana na tajiri na mmiliki wa klabu hiyo mrusi Roman Abramovich japo ameendelea kubaki katika historia ya klabu ya timu hiyo kuwa kocha aliyeiletea vikombe vingi klabu hiyo.

Hata hivyo tetesi zimezidi kuzagaa kwamba Mourinho anarejea Chelsea baada ya kocha wa sasa wa Chelsea Rafael Benitez kusema kwamba ataondoka Chelsea mwishoni mwa msimu huu

"Ninapendwa na mashabiki na vyombo vya habari ambao wananitendea haki ,ninajua Hispania ni tofauti kwasababu watu wengi wananichukia" Alisema Mourinho.
Chelsea fans' banner

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!