Searching...
Jumamosi, 5 Julai 2014

MOURINHO AIFANYIA UMAFIA R.MADRID,AMZIDI KETE ANCHELOTI KIUNGO WA BAYERN


  JOSE MOURINHO
Kocha wa Chelsea Mreno Jose Mourinho amefanya umafia baada ya kuingilia kati uhamisho wa mchezaji kiungo mshambulaji wa Bayern Munich Toni Kross kwenda Real Madrid baada ya jana jana usiku kupeleka ofa nono ya zaidi ya paundi milioni 25 zilizoahidiwa na Madrid,kitita ambacho kinailazimu Bayern Munich kuvunja mazungumzo na Real Madrid na taarifa zinasema uhamisho huo unaweza ukakamilika ndani ya saa 48 zijazo.
TONI KROSS
Bayern Munich wanalazimika kumuuza kiungo huyo huku bado udenda ukiwatoka kufuatia mchezaji  huyo kugoma kuongeza mkataba na Bayern Munich msimu huu;japo aliombwa asaini na ataongezewa mshahara lakini bado akagoma.

Kroos mbaye ameisaidia timu yake ya taifa ya Ujerumani alishasema wakati wa michuano ya kombe la dunia hatozungumza na klabu yoyote na wala waandishi wa habari kuhusu uhamisho kwani anahitaji kujikita zaidi kuisaidia timu yake na mambo mengine yatafuata baada ya michuano.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!