LOUIS VAN GAAL.
Kocha mpya wa Manchester United Louis van Gaal pamoja na kwamba yupo kwenye michuano ya kombe la dunia lakini ameonekana kuwatia matumbo joto makocha wa ligi kuu England hasa wa timu za Man City,Chelsea,Liverpool,Arsenal na Tottenham kutokana na speed yake ya usajili na aina pia ya wachezaji anaowanunua.
DE JONG.
kwa sasa Gaal ameelekeza nguvu zake kwa kiungo wa zamani wa City ambaye kwa sasa anakipiga na klabu ya AC Milan YA Italia Nigel de Jong.
Baada ya United
kumnasa kiungo Ander Herrera, sasa Van Gaal anataka kumuongezea nguvu ili kumpata mtu wa kusaidiana naye kumiliki mipira katikati na kusukuma mashumbulizi kwa nguvu, na De Jong anaonekana kuwa chaguo sahihi la Van Gaal.
Wachambuzi wa mambuzi wa soka wanasema kuja kwa kocha Louis Vana Gaal kunako ligi kuu ya England kutaamsha msisimko mkubwa katika ligi hiyo msimu ujao ambapo tayari makocha wenzake kama Mourinho na Wenger wanaonekana kuanza kuweweseka kutokana na usajili anaoufanya Van Gaal.
TOA MAONI YAKO HAPO CHINI UKIANDIKA PIA JINA LAKO NA KISHA SHARE KWA MARAFIKI ZAKO.
0 comments:
Chapisha Maoni