NEMANJA VIDIC.
Nemanja, beki mwenye nguvu, shupavu, shujaa na kiongozi uwanjani, amebwaga manyanga baada ya miaka minane ya kukipiga Old Trafford na amekiri kwamba ataondoka mwishoni mwa msimu huu.
Nemanja, beki mwenye nguvu, shupavu, shujaa na kiongozi uwanjani, amebwaga manyanga baada ya miaka minane ya kukipiga Old Trafford na amekiri kwamba ataondoka mwishoni mwa msimu huu.
Mbabe huyo wa kimataifa wa Serbia ameichezea
Manchester United tangu mwaka 2006, lakini hataendelea kuwapo tena
klabuni hapo mara baada ya msimu huu mkataba wake utakapomalizika rasmi.
“Sifikirii kubaki England kwa sababu klabu pekee
ambayo nilitaka kuichezea hapa ni Manchester United. Sikuwahi kufikiria
kama ningetwaa mataji 15. Hata hivyo nimeamua kuondoka mwishoni mwa
msimu. Nataka kujipa changamoto mpya,” alisema Nemanja katika taarifa
rasmi aliyoituma katika mtandao wa klabu yake.
Vidic, ambaye uhamisho wake wa Pauni 7 milioni
kutoka Spartak Moscow kwenda Old Trafford ulitangazwa siku ya Krismasi
ya mwaka 2005, alikuwa nahodha wa Manchester United wakati ilipotwaa
taji la 20 la Ligi Kuu England kihistoria msimu uliopita chini ya kocha
Alex Ferguson.
“Nimekuwa na miaka minane ya kushangaza sana hapa.
Muda wangu katika klabu hii kubwa siku zote utazungumzwa kama muda bora
wa maisha yangu ya soka,” aliongeza.
“Sitausahau usiku ule mzuri Moscow (wakati Man
United ikiichapa Chelsea na kutwaa ubingwa wa Ulaya mwaka 2008), ni
kumbukumbu nitakazoishi nazo kwa miaka yote nitakayoishi hapa duniani.”
Vidic aliichezea Manchester United kwa mara ya
kwanza Januari 25, 2006 katika pambano la Ligi Kuu England dhidi ya
Blackburn Rovers na kuanzia hapo alitwaa mataji matano ya ligi hiyo,
moja la Ligi ya Mabingwa Ulaya na matatu ya Kombe la Ligi.
Inadaiwa kwamba tayari beki huyo ana makubaliano
ya kujiunga na Galatasaray ya Uturuki kwa mshahara mnono huku
akitarajiwa kujiunga na wakali wengine waliowahi kukipiga Ligi Kuu
England kama vile Didier Drogba na Emmanuel Eboue.
Itakumbukwa kuwa uhusiano wake wa muda mrefu wa
uwanjani na beki mwingine wa United, Rio Ferdinand, ambaye pia
anatarajiwa kutangaza kutundika daruga muda wowote kuanzia sasa.
Hii ni moja ya picha zilizotumwa kwenye mitandao ya kijamii na wapenzi wa klabu ya Manchester United wakimnanga kocha wao Moyes kwamba anawaacha makamanda wake Nemanja Vidic na Van persie kutimka huku jahazi la klabu hiyo likizama.
Hii ni moja ya picha zilizotumwa kwenye mitandao ya kijamii na wapenzi wa klabu ya Manchester United wakimnanga kocha wao Moyes kwamba anawaacha makamanda wake Nemanja Vidic na Van persie kutimka huku jahazi la klabu hiyo likizama.

0 comments:
Chapisha Maoni