Searching...
Jumatano, 8 Januari 2014

TETESI ZA UHAMISHO DIRISHA DOGO ULAYALIVERPOOL,MAN U,TOTTENHAM KUZIDIWA KETE NA ZENIT



 Lamela wants to quit Spurs, says dad Jose
 ERIK LAMELA.
Mchezaji wa Tottenham Erik Lamela anaonekana kufikia ukingoni kukipiga na miamba hiyo ya soka baada ya baba yake kuweka wazi kwamba mwanae anataka kuondoka White Hart Lane. Mshambuliaji huyo alijiunga na Spurs msimu uliopita kwa kitita kikubwa cha paundi milioni 30 na kuweka rekodi klabuni hapo.
 Loan target: Arsenal are keen on a short-term deal for the Real Madrid forward Alvaro Morata, seen here after scoring against Levante back in October
 ALVARO MORATA.
Arsenal wanaonekana kuongeza juhudi za kuipata saini ya mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 21, kwa mkopo wa muda mrefu.
SUPER MARIO BALOTELLI.
Mshambuliaji mtukutu wa AC Milan super Mario Balotelli, 23, ametupilia mbali na kupuuzia taarifa zinazoenezwa na vyombo mbalimbali vya habari Italia kwamba ana mpango wa kuihama timu yake mwezi huu.
 
NEMANJA VIDIC.
Beki kisiki wa Manchester United Nemanja Vidic amesema anataka kuondoka Old Trafford mwishoni mwa mwa msimu huu,kwa sasa Vidic amesalia na mkata wa miezi sita tu kunako Manchester United na wakala wake amesema tayari anazo ofa nzuri za timu za Italia Serie A lakini hakuitaja ni timu gani japo watu wanadai anataka kutimkia Inter au Ac Millan.
 
ANDREA PIRLO
Kiungo mkongwe Andrea Pirlo 34 yupo tayari kuingia mkataba mpya wa miaka miwili na timu yake ya kibibi kizee cha Turin Juventus.
 
JAY BOTHROYD
Mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya England na Queens Park Rangers mshambuliaji Jay Bothroyd amesaini kandarasi ya paundi  milioni 5 kukipiga na tumu ya  Muangthong United ya nchini Thailand.
MOHAMED SALAH.
Timu ya Zenit St Petersburg ua Urusi ipo mbioni kuwazidi kete Liverpool, Manchester United na Tottenham kuinasa saini ya mshambuliaji wa timu ya Basle Mohamed Salah 21.
 
CRAIG GARDNER.
West Bromwich Albion wanataka kumsajili kiungo wa Sunderland  Craig Gardner,kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 anamaliza mkataba wake mwishoni mwa msimu huu ambapo kama hawatamuuza sahivi basi ataondoka bure mwishoni mwa msimu.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!