Hapana shaka wapenzi wa soka barani Afrika pamoja na
kuomboleza kifo cha Nelson Mandela wamekuwa wanafuatilia Droo ya kombe
la dunia kufahamu nani wapinzani wa timu tano zinazowakilisha bara hilo.
Cameroon wamejikuta katika kundi gumu la A pamoja na wenyeji Brazil, Mexico na Croatia.
Mabingwa watetezi Uhispania watakuwa
katika kundi B pamoja na Netherlands waliokutana nayo fainali kombe
lililopita, na timu zingine ni Chile na Australia.
Dua ya Ivory Coast ya kuepuka kundi gumu sana
wakati huu inaonekana imesikika, wako katika kundi C pamoja na Colomboa,
Japan na Ugiriki.
KOCHA WA ENGLAND ROY HODGSON.
England watakuwa na kibarua kigumu kwenye kundi D ambapo wapinzani wao ni Italia, Uruguay na Costa Rica.
Kwenye kundi E Ufaransa inacheka usiku huu kwani
imepangwa pamoja na Uswizi, Ecuador na Honduras.Mabingwa wa Afrika
Nigeria wako katika kundi F pamoja na Argentina Iran na Bosnia
Harcegovinia, ambayo inashiriki kombe la dunia mara ya kwanza.
Ghana ndiyo inayoonekana kuwa matatizoni
miongoni mwa timu za Afrika. Wamejikuta katika kundi G ambapo watapamaba
na na Ujerumani, Marekani na Ureno.Timu ya tano ya Afrika Algeria
itakuwa kwenye kundi H na wapinzani hapo ni Ubelgji, Korea Kusini na
Urusi.
MAKUNDI KAMILI HAYA HAPA.
Group B: Spain, Chile, Australia, Holland
Group C: Colombia, Ivory Coast, Japan, Greece
Group D: Uruguay, Italy, Costa Rica, England
Group E: Switzerland, Ecuador, Honduras,France
Group F: Argentina, Nigeria, Iran, Bosnia
Group G: Germany, Ghana, USA, Portugal
Group H: Belgium, Algeria, South Korea, Russia
0 comments:
Chapisha Maoni