Searching...
Jumamosi, 7 Desemba 2013

ANGALIA PICHA MBALI MBALI ZA MZEE MADIBA ZIKIAMBATANA NA HISTORIA YAKE.

Mandela mwaka 1956
Nelson Mandela alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mwafrika mweusi wa Afrika Kusini,baada ya vita vya muda mrefu dhidi ya utawala wa kizungu. 
Alizaliwa mkoani Eastern Cape, lakini baadaye akatorokea mjini Johannesburg ambako alifanikiwa kuwa Wakili na kujiunga na haratakati za chama cha ANC dhidi ya utawala wa kizungu.  
 -9b362eff4ab20164

Kama kijana, Mandela alipenda masumbwi. ''Masumbwi ni bure, Ukiwa ulingoni , umri na hadhi yako pamoja na mali yako sio muhumu,'' aliandika katika kitabu chake kuhusu maisha yake.
 
 Mwaka 1956, alituhumiwa kwa kosa la uhaini kwa sababu ya kazi yake na ANC. Wakati wa kesi yake, alikutana na mfanyakazi wa kijamii aliyeitwa, Winnie Mandela. Ndao yake kwa Evelyn Mase iliisha baada ya wawili hao kutalakiana. 
 Nelson na Winnie walioana mwaka 1958 lakini hawakufurahia maisha yao ya ndoa kwani wote walikuwa wakikamatwa mara kwa mara. 
 Kufuatia kesi ya pili ya uhaini dhidi ya Mandela, alifungwa maisha jela mwaka 1964.
Kampeini ya kimataifa ilianza dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi. Licha ya Afrika Kusini kuwekewa vikwazo vya kiuchumi, ingawa havikuwa vikali, wasanii mashuhuri na wananchi wa kawaida kote duniani waliendelea kushinikiza,Sura ya Mandela ikawa sasa iishara ya kampeini hiyo kote duniani.
Hatimaye zaidi ya miaka ishirini baada ya kufungwa jela, Mandela aliachiliwa mwaka 1990.

Kufuatia kuachiliwa kwake, Mandela lizuru nchi nyingi na kukutana na viongozi wa dunia alipokuwa njiandaa kuwania urais. Anaonekana hapa katika ubalozi wa Afrika Kusini mjini London ambako maandamano ya kupinga utawala wa kizungu daima yalikuwa yakifanyika.  
Mashauriano makubwa yalifanyika kabla ya rais FW de Klerk kukubali au kuruhusu watu kupiga kura. Wawili hao walituzwa tuzo ya amani ya Nobbel, kwa sababu ya kumaliza ubaguzi wa rangi Afrika Kusini. 

Uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia ulifanyika tarehe 27 mwezi Aprili m,waka 1994. Waafrika weusi walipanga foleni kupiga kura kwa mara ya kwanza. Chama cha ANC kilishinda uchaguzi huo kwa wingi wa kura na hivyo Mandela kuwa rais wa kwanza mweusi kuongoza Afrika Kusini .
 Mandela alitawala nchi hiyo kwa muhula mmoja pekee na mnamo mwaka 1999 akawa mmoja wa viongiozi wachache wa Afrika kuachia ngazi kwa hiari. Thabo Mbeki, alipewa jukumu la kumrithi Mandela kama rais na kiongozi wa ANC.
Mzee Madiba pia aliweza kuonekana na mitindo ya kipekee kwa sababu ya T sheti zake nzuri nzuri. Hapa anawaluiza wandishi wa habari maoni yao kuhusu shati yake, baada ya maankuli ya mchana na muundajji wa mitindo Pierre Cardin  


Pia ana mambo mawili ambayo sio kawaida kwa viongozi wa dunia kuwa nayo....mpole na mwenye kuweza hata kujicheka , hapa anakutana na mwanamfalme Prince Charles na wanamuziki wa iliyokuwa bendi ya Spice Girls.
Baada ya kutalakiana na mkewe Winnie , Mandela alimuoa Graca Machel, alipokuwa anasherehekea miaka 100m mwaka 1998. Bi Machel ni mjane wa aliyekuwa rais wa Msumbiji Samora Machel. Bi Graca na Mandela walianzisha hazina ya kuwasaidia watoto wasio na uwezo mkubwa maishani  .


Tangu kuondoka mamlakani, mwaka 1999, bwana Mandela alikuwa mmoja wa viongozi wakuu kufanya kampeini dhidi ya ukimwi na utovu wa usalama wakati nchi yake ilipokuwa mwenyeji wa kombe la dunia mwaka 2010.
 
Mwaka 2004, akiwa na umri wa miaka 85, Mandela alistaafu kutoka majukumu ya umma ili kuwa na muda na faimlia yake pamoja na marafiki zake.  

pele

Bwana Mandela, aliweza kujitokeza wakati wa sherehe ya kufunga michuano ya kombe la dunia mwaka huo. Hali yake ya kiafya ilikuwa mbaya na alikuwa anaomboleza kifo cha kitukuu wake aliyeuawa huku michuano hiyo ikianza. 

Kwaheri Baba wa Afrika daima milele dumu tutakukumbuka.
,

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!