Searching...
Ijumaa, 25 Oktoba 2013

HILI NDILO GARI LA MAITI LILILOTEKWA NA MAJAMBAZI NA KUBOMOA JENEZA NA KUPORA FEDHA

 Gari aina ya Land cruiser mali ya chuo cha SUA cha mjini Morogoro kama linavyoonekana baada ya kupigwa mawe na watu wanaodhaniwa kuwa ni majambazi  nje kidogo ya mji wa Singida.
 Kesi inayowakabili washitakiwa watano walioteka gari la chuo cha SUA mjini Morogoro na kunyang’anya zaidi ya shilingi 19.8 milioni, hukumu yake inatarajiwa kutolewa kesho na mahakama ya wilaya ya Singida. Utekaji huo ulifanyika Desemba sita mwaka jana saa saba na nusu usiku kwenye barabara kuu ya Dodoma – Singida eneo la Kisaki manispaa ya Singida.
Hudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya mkoa mjini Singida ambaye jina lake halikuweza kutambuliwa mara moja,akiliweka sawa baada ya kufanyiwa ukarabati baada ya kubomolewa na majambazi na kulisachi.
KESI inayowakabili washitakiwa watano ya utekaji wa gari la chuo cha SUA Morogoro mjini na kisha kunyang’anya zaidi ya shilingi 19.8 milioni hukumu yake inatarajiwa kutolewa kesho na Mahakama ya Wilaya ya Singida.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!