MBUNGE WA CHADEMA APAMBA MKUTANO WA CCM MEATU,AWAMWAGIA SIFA KINANA NA NAPE
Home
»
Unlabelled
» MBUNGE WA CHADEMA APAMBA MKUTANO WA CCM MEATU,AWAMWAGIA SIFA KINANA NA NAPE
Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza
Mbunge wa CHADEMA jimbo la Maswa Magharibi Mh. John Shibuda wakati
akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya
Meatu mjini Meatu, ambapo ameelezea kuwa Siasa siyo ugonvi na alikuja
Meatu kwa sababu mbili tu Moja ilikuwa ni kukutana na Ndugu Kinana kwa
ajili ya kujadiliana mambo mbalimbali juu ya tatizo la zao la Pamba
kuhusu bei ya zao hilo na matatizo ya pembejeo kwa wakulima wa Wilaya
hiyo, Akaaongeza kwamba jambo la pili ni kwamna Ndugu Abdulrahman Kinana
ni rafiki yake wa muda mrefu kwa hata wakati wakisoma shule wote
walisoma moshi Abdulrahman Kinana akisoma Old Moshi Sekondari na John
Shibuda Mwenyewe akisoma Moshi Technical lakini pia akasema wakati
alipokuwa akigombea ubunge wa Maswa Magharibi Kinana alimchangia
shilingi Milioni moja "Siasa nia Siyo Matusi ni Ushirikiano na kukosoana
kwa hoja" amemaliza Shibuda. Katibu
Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza
jambo katika mkutano huo huku Mbunge wa jimbo la Maswa Magharibi John
Shibuda akimsiliza, kushoto anayetabasam ni Katibu wa NEC Itikadi,
Siasa na Uenezi Nape Nnauye.
Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akizungumza katika
mkutano huo kushoto ni John Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi
CHADEMA.
Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi Nape Nnauye akikumbatiana kwa
furaha na John Shibuda Mbunge wa Jimbo la Maswa Magharibi CHADEMA mara
baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya Meatu mjini, kushoto ni
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishuhudia. Mbunge
wa Jimbo la Maswa Magharibi CHADEMA Mh John Shibuda akiwasili katika
mkutano wa hadhara wa Chama cha Mapinduzi uliofanyika kwenye viwanja vya
Meatu mjini Meatu leo huku vijana wa Chama chaCHADEMA wakimsindikiza..
0 comments:
Chapisha Maoni