Searching...
Ijumaa, 20 Septemba 2013

KIFO CHA ZAO LA PAMBA HIKI HAPA

Meneja wa kiwanda cha Bilchand Oil Mill, Mohamed Gupta akifafanua uchafuzi unaofanywa na baadhi ya wanunuzi na wakulima kwa kuchang’anya pamba, maji, mchanga na mbegu kwa lengo la kuongeza uzito.
Ziara ya Mwenyekiti wa Bodi ya Pamba nchini DKT.FESTUS LIMBU katika kiwanda cha kuchambua pamba cha Birchand Oil mill inayomwezesha kujionea uchafuzi wa pamba unaofanywa na baadhi ya wanunuzi na wakulima kwa kuchang’anya pamba, maji, mchanga na mbegu kwa lengo la kuongeza uzito.
Mbegu zilizochanganywa kenye pamba kwa lengo la kuongeza uzito
Ukaguzi ukiendelea kwenye ghala la Pamba.
Meneja wa kiwanda cha Bilchand Oil Mill, Mohamed Gupta akionyesha mchanga uliochanganywa na Pamba za moja wa wakulima waliokiuzia kiwanda chake.
Ukiitizama kwa harakaharaka pamba hii unaweza kuiona kuwa iko salama, ila ukichukuwa jukumu la kuigusa ndipo utagunduwa kuwa kunachembe chembe za mchanga na uchafu mwingine ndani yake.
Hili ni lundo la mchanga wa kilo 60,000 uliopembuliwa wakati wa uchambuzi wa pamba ya msimu huu na uliopita, kwa Kiwanda cha Bilchand Oil Mill ambacho kimepata hasara ya zaidi ya shilingi milioni 7 kutokana na uchafuzi huo wa kuweka maji na mchanga, hadi sasa Wahasibu wake wanne (hakuwataja) wafikisha polisi kwa tuhuma hizo.  
Meneja wa kiwanda cha Bilchand Oil Mill, Mohamed Gupta akielezea uchafuzi huo ndani ya Pamba.
Kwa ukaribu zaidi mchanga uliopatikana kwenye Pamba baada ya uchambuzi wa awali.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!