Kutoka
kushoto ni Tatu Issa mwanafunzi wa chuo kikuu cha SAUTI tawi la Songea ,
Tamimu Adam mtangazaji wa Radio Jogoo FM na Aneth Mponda mwanafunzi wa
chuo kikuu cha SAUTI tawi la songea wakiwa wanajadili mada inayohusu
matumizi ya mitaandao ya kijamii katika kipindi cha Jamvi letu
kinachoendesha na kituo hicho cha radio katika manispaa ya songea Mkoani
Ruvuma'
Aneth akielezea faida anayoipata kupitia mitandao ya kijamii hasa
Facebook ambayo kwake ni rahisi kutumia ikiwa ni kubadilishana mawazo
ila kwa upande wa Twitter kwake inamuwia ngumu kuitumia kutokana na
ilivyo , kwa upande wa changamoto anazokutana nazo amesema " kuna watu
humu katika mitandao hutumia sivyo mara kwa mara unakuta wanakutaka
kimapenzi na ukimkatalia bado hakomi kila akikuona upo hewani lazima
akutumie ujumbe wa mapenzi wakati umemkatalia yeye anakung'ang'nia pia
kuna baadhi huweka picha za ngono amabazo ni kinyume na maadili ya
kiTanzania unakuta ni mtu mzima na haendani na matendo anayoyafanya pia
kuana wengine hawajiamini wanaweka picha si zao " alisema.
Tamimu Adam akisikiliza kwa makini mawazo toka kwa washiriki wa kipindi cha Jamvi letu
Tatu
Issa akielezea faida ya matumizi ya mitandao ya kijamii kwa upande
wake ni kupata taarifa mbalimbali pia kubadilishana mawazo na marafiki
mbali mabali na kupata marafiki kupitia mitaandao pia kwa siku anasema
anaingia mara mbili na hutumia zaidi ya masaa matatu na moja ya mtandao
anaopenda ni facebook .
"
Japo natumia mitandao hii ya kijamii lakini bado siiyamini kwani kuna
baadhi huweka habari zisizo za ukweli mfano kuhusu mitandao ya kijamii
iliyozusha juu ya kifo cha msanii Saida kaloli " alisema
0 comments:
Chapisha Maoni