Mshambuliaji mwenye kipaji kisichochujuka mreno Christian Ronaldo amekanusha vikali kuhusu uvumi unaovumishwa kila kukicha navyombo vya habari kwamba amesaini mkataba mpya na klabu yake ya Real Madrid kwamba sio kweli,kauli iliyopokelewa kwa mikono miwili na vilabu mbalimbali vinavyomuwania winga huyo ambaye inasemekana kwamba kwa sasa hafanyi kazi kwaajili ya hela bali kwaajili ya amani na furaha ya familia yake ambapo tetesi zinasema familia yake inapenda arejee England ambapo sasa Manchester United na Chelsea wameamka upya kupigania saini ya mreno huyo....Christian Ronaldo amesema zaidi ya watu 5,656 marafiki zake kwenye facebook wamependa ujumbe wake kwenye facebook
Huo ndio ujumbe aliouandika Ronaldo kwenye ukurasa wake wa facebook.
ANDRE SCHURRLE.
Andre Schurrle ametajwa kuwa mchezaji wa kwanza kusainishwa na kocha wa chelsea mreno Jose Mourinho tangu atue klabuni hapo kutokea Madrid.
The Blues wamekubaliana na klabu ya Bundesliga ya Bayer Leverkusen ya ujerumani paundi milioni 18 ili kumnasa mshambuliaji huyo aliyewatesa sana Barcelona katika mechi za klabu bingwa ulaya msimu uliopita
Schurrle, 22,amesema sasa kilichibaki ni maelewano yake binafsi na klabu ya chelsea na kisha kuchukuliwa vipimo kabla ya kuhitimisha uhamisho huo.
"Chelsea na Bayer
Leverkusen wameshafikia makubaliano ya uhamisho wa mchezaji Andre
Schurrle," mtandao wa klabu hiyo unaeleza
0 comments:
Chapisha Maoni