Searching...
Jumamosi, 22 Juni 2013

BARAZA LA MADIWANI MBINGA LAGAWANYIKA NA KUZAA NYASA

 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu akizungumza katika kikao cha uvunjaji wa baraza la madiwani wa wilaya ya Mbinga leo hii katika ukumbi wa Maendeleo.
 Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu akionyesha hati za utambulisho wa Halmashauri mbili za nyasa na mbinga kabla yta kukabidhi hati hizo
 Mkurugenzi wa Wilaya ya Nyasa Shaib Mnunduma akipokea hati ya utambulisho wa Halmashauri ya wilaya ya Nyasa
Toka toka kushoto kwako aliyekaa ni mkuu wa Wilaya ya Mbinga Senyi Ngaga na aliyesimama ni  Mkurugenzi mpya wa Halmashauri ya Wilaya Mbinga Hussen Ngaga akizungumza jambo wakati wa Baraza la madiwani wa Halmashauri hiyo kabla ya kuvunjwa.
 Mkuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi akizungumza baada ya kutangazwa na mkuu wa Mkoa wa Ruvuma  Said Thabiti Mwangu  kuvunjwa  Baraza la madiwani  wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga
Baadhi ya wataalam wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga na Nyasa wakisikiliza nasaha za viongozi Mbalimbali kabla ya kuvunjwa kwa Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Mbinga kufuatia kuzaliwa kwa Halmashauri mpya ya Nyasa.
 Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga ambayo imezaa Halmashauri mpya ya Nyasa wakimsikiliza mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Said Thabiti Mwambungu alipokuwa akitoa nasaha zake wakati wa uvunjaji wa Balaza la madiwani.
-----------------------------------------
Na Nathan Mtega,Mbinga

HATIMAYE baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkoani Ruvumalimegawanyika baada ya mchakato wa kuanzishwa kwa halmashauri mpya ya wilaya ya Nyasa na kupatikana kwa wakurugenzi wa halmashauri hizo mbili na kukabidhiwa hati za utambulisho wa halmashauri zilizokabidhiwa kwa wakurugenzi wa halmashauri hizo na mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu baada ya kuvunjwa kwa baraza hilo.



Akizingumza katika kikao hicho cha dharula cha baraza la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Mbinga mkuu wa mkoa wa Ruvuma Said Mwambungu mbali ya kulipongeza baraza hilo la madiwani lililokuwa linagawinyika kwa ajili ya kuanzishwa kwa baraza jipya la halmashauri ya wilaya ya Nyasa amesema kuwa maendeleo na mafanikio makubwa yaliyopo katika halmashauriya wilaya ya Mbinga yametokana na ushirikiano uliokuwepo baina ya madiwani hao pamoja na wataalamu hivyo unapaswa kuendelezwa kwa pande zote mbili.


Amesema mgawanyiko huo unapaswa kuwa kichocheo cha maendeleo ya kwa pande hizo mbili ambazo zimegawanyika kwa kufuata kanuni na sheria zilizopo bila kutokea hitilafu yoyote katika mgawanyo wa mali, watumishi pamoja naadeni yaliyopo hali inaonyesha ukomavu wa viongozi pamoja na wataalamu wao ambao kwa pamoja waliifanya halmashauri ya wilaya ya Mbinga kuwa na sifa kubwa ya uzalishaji na ukusanyaji wa mapato ya ndani.


Aidha amewataka wakurugenzi watendaji wa halmashauri hizo mbili kuhakikisha watumishi waliopangwa kwenye halmashauri hizo baada ya mgawanyo huo kuwa wameripoti kwenye  vituo vyao vya kazi ifikapo Julai mosi mwaka huu bila kuwepo kwa visingizio vya aina yoyote kwa sababu wanapaswa kuheshimu mabadiliko hayo yaliyofuata taratibu na kupewa baraka na uchaguzi wa wenyeviti na viongozi wengine kwenye halmashauri hizo unapaswa kuwa umefanyika katika kipindi hicho bila kutokea vurugu yoyote.


Alisema kuwa halmashauri ya wilaya ya Mbinga imekuwa ikipata hati safi  ikiwa na baraza la madiwani 48 kablaya mgawanyo huo na hati hizo zilipatikana kwa ushirikianomzuri uliokuwepo hivyo hati safi hizo zitaendelea kwa pande zote mbili ambazo awali zilikuwa pamoja na ushirikiano unapaswa kudumishwa kwa ajili ya maslahi na maendeleo ya wananchi wa halmashauri  hizo.


Amesema kuwa serikali kuu itatoa ushirikiano wa karibu kwa halmashauri mpya ya Nyasa ili kuhakikisha inapiga hatua kimaendeleo na kuweza kutoa huduma bora kwa wananchi huku akiwataka wakururugenzi wa halmashauri hizo Shaib Mnunduma(Nyasa) na Hussein Issa(Mbinga) kuendelea kutoa ushirikiano kwa madiwani.


Wakizungumza baada ya mkuu wa mkoa wabunge wawili wa wilaya hizo mbili Kapten  John Komba na Gaudens  Kayombo mbali ya kupongeza uamuzi wa serikali kukubali ombo lao hilo la muda mrefu la kuwepo kwa mgawanyo wa wilaya na halmashauri lakini pia waliwataka madiwani na wataalamu kwenye halmashauri hizo kuendeleza ushirikiano wa karibu uliokuwepo kwa ajili ya maslahi ya wananchi wanaowaongoza.


Aidha nao wakuu wa wilaya ya Nyasa Ernest Kahindi wa Nyasa na  Senyi Ngaga wa Mbinga kwa pamoja walishauri kuwepo kwa ushindani wa kimaendeleo kw ajili ya wananchi na si vinginevyo kwa sababu wilaya ya Mbinga haina utamaduni wa migogoro inayorudisha nyuma jitihada za wananchi katika kujiletea maendeleo yao.
HABARI KWA HISANI YA DEMASHO BLOG.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!