MASAA zaidi ya 6 ya
mapambano kupiga mabomu ya machozi na
kurushiana mawe kati ya
wafanyabiashara ndogo ndogo (machinga) na askari
wa kikosi cha kutuliza
ghasia (FFU) mkoani Iringa
yaishia pabaya kwa jeshi la
polisi kumkamata mbunge wa
jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa (chadema) na
watu wengine zaidi ya 60
Polisi watumia mabom ya machozi kutawanya machinga wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi abiria
walazimika kutimua mbinu na kuacha mizigo yao katika magari huku machinga hao wakitumia mawe na kuchoma mataili moto barabarani kuvunja vioo vya gari la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama njia ya
kupambana na polisi
Tukio hilo la Mapambano kati ya machinga na polisi lilitokea leo kuanzia muda wa saa 3 asubuhi
na kuendelea hadi saa 8 mchana katika eneo la Mashine tatu
mjini Iringa na maeneo mbali
mbali ya mji wa Iringa
Hata hivyo alisema wao kama walalahoi wanampongeza mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo haungi mkono njia inayotumiwa na mbunge ya kuwahamasisha kuvunja sheria na kuwa matatizo na majeraha wanapata wao wananchi na sio mbunge.
Awali mbunge
mchungaji Msigwa kabla ya kukamatawa na
jeshi la polisi alitoweka katika
mazingira tata katika eneo hilo la mashine tatu na
kuibukia eneo la chuo kikuu cha
Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee
ya kuchangia Kanisa na mgeni rasmi akiwa
waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara baada ya
shughuli hiyo kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na
kufikishwa kituo cha polisi.
Kabla ya
kukamatwa kwake mbunge Msigwa
alizungumza na mwandishi wa habari hizi
na kuwa yupo tayari kukamatwa wakati
wowote na kuwa kamwe ataendelea
na msimamo wake wa
kuwataka Machinga kufanya biashara
eneo hilo.
Mbali ya
kukamatwa kwa mbunge
Msigwa kwa kuhusishwa na vurugu hizo pia
jeshi la polisi mkoani Iringa
linawashikilia watu wengine
zaidi ya 60 akiwemo aliyekuwa
kampeni meneja wa Chadema jimbo la Iringa mjini na mgombea udiwani
kata ya kwa Kilosa Abuu Changawa Majeck.
Huku idadi ya
majeruhi waliojeruhiwa kwa kupigwa mawe na machinga na badhi ya machinga waliokamatwa kwa vurugu
hizo pia wakijeruhiwa vibaya wakati
wakipambana na polisi hao.
Taarifa kutoka jeshi
la polisi zilizothibitishwa na kamanda
wa polisi mkoa wa Iringa Michael
Kamuhanda zinadai kuwa
watu zaidi ya 60 ndio wamekamatwa
hadi sasa na jitihada za
kuwasaka wengine waliohusika
katika vurugu hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa
mali za
wananchi unaendelea.
Huku akidai mali mbali mbali
zimeharibiwa likiwemo gari hilo
la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu
mwingine mdogo mdogo
wa mali za wananchi
Jeshi hilo la
polisi limesema kamwe halipo tayari kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo
atakapofikishwa mahakamani Kesho
|
Jumatatu, 20 Mei 2013
Related Posts
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 comments:
Chapisha Maoni