Na Francis Godwin, Iringa
MASAA  zaidi ya 6 ya mapambano kupiga  mabomu ya machozi na kurushiana  mawe kati ya wafanyabiashara  ndogo  ndogo (machinga) na  askari  wa  kikosi cha  kutuliza  ghasia (FFU) mkoani Iringa  yaishia pabaya  kwa  jeshi la  polisi kumkamata  mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa  (chadema) na  watu  wengine zaidi ya 60
Polisi  watumia  mabom ya machozi  kutawanya machinga  wapiga mabomu hadi stendi kuu ya mabasi  abiria  walazimika  kutimua  mbinu na kuacha mizigo  yao katika magari   huku machinga  hao wakitumia mawe  na kuchoma mataili  moto barabarani  kuvunja vioo vya gari  la Zimamoto na kuharibu mali mbali mbali kama  njia ya  kupambana na  polisi
 Tukio hilo la Mapambano  kati ya machinga na polisi lilitokea leo  kuanzia  muda wa saa 3  asubuhi  na kuendelea  hadi saa 8 mchana katika  eneo la Mashine  tatu  mjini  Iringa na maeneo mbali mbali ya mji  wa Iringa


Hata   hivyo  alisema wao kama walalahoi wanampongeza  mbunge wao kwa kuonyesha kuwapigania japo haungi mkono njia  inayotumiwa na mbunge ya  kuwahamasisha   kuvunja  sheria na kuwa  matatizo na majeraha  wanapata  wao  wananchi  na sio mbunge.
Awali  mbunge mchungaji Msigwa  kabla ya  kukamatawa na  jeshi la  polisi alitoweka katika mazingira  tata katika  eneo hilo la mashine  tatu na  kuibukia eneo la chuo  kikuu cha Tumaini Iringa ambako kulikuwa na harambee  ya  kuchangia Kanisa na mgeni  rasmi akiwa  waziri mkuu mstafu Frederick Sumaye na mara  baada ya  shughuli  hiyo  kumalizika ndipo alipokamatwa na polisi na kufikishwa  kituo cha  polisi.
Kabla ya  kukamatwa  kwake mbunge Msigwa alizungumza na mwandishi  wa habari hizi na kuwa  yupo tayari kukamatwa  wakati  wowote na  kuwa kamwe  ataendelea  na msimamo  wake  wa  kuwataka Machinga  kufanya  biashara  eneo hilo.
Mbali ya  kukamatwa  kwa  mbunge  Msigwa  kwa  kuhusishwa na vurugu  hizo pia  jeshi la  polisi  mkoani Iringa  linawashikilia  watu  wengine  zaidi ya 60 akiwemo  aliyekuwa kampeni meneja  wa Chadema  jimbo la Iringa mjini na mgombea  udiwani  kata ya  kwa Kilosa  Abuu Changawa Majeck.
Huku  idadi ya majeruhi  waliojeruhiwa kwa  kupigwa mawe na machinga na  badhi ya machinga  waliokamatwa kwa  vurugu  hizo pia wakijeruhiwa  vibaya  wakati  wakipambana na  polisi hao.

Taarifa  kutoka  jeshi  la polisi zilizothibitishwa na kamanda  wa polisi mkoa  wa Iringa Michael Kamuhanda  zinadai  kuwa  watu  zaidi ya 60 ndio  wamekamatwa  hadi  sasa na  jitihada za  kuwasaka wengine  waliohusika katika  vurugu  hizo ambazo zimesababisha uharibifu mkubwa wa mali  za  wananchi unaendelea.
Huku akidai  mali  mbali mbali  zimeharibiwa likiwemo gari  hilo la zimamoto mjini Iringa pamoja na uharibifu  mwingine  mdogo  mdogo  wa mali za  wananchi
Jeshi  hilo la polisi  limesema kamwe halipo tayari  kumwachia mbunge Msigwa kwa leo hadi hapo atakapofikishwa mahakamani Kesho