Searching...
Alhamisi, 30 Mei 2013

KINANA NA UJUMBE WAKE WAKAGUA HALI YA USALAMA NA AMANI HUKO ZIWA NYASA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (mbele) akiwa na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Njombe, Deo Sanga, wakikagua hali ya usalama na amani katika mwambao wa Ziwa Nyasa eneo la Lupingu wakati wa ziara ya kikazi ya siku saba ya kuimarisha uhai wa chama hicho mkoani Njombe leo. 
PICHA ZOTE NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA
  Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (wa pili kulia) akiwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (mbele) wakikagua hali ya usalama na amani katika mwambao wa Ziwa Nyasa eneo la Lupingu wakati wa ziara ya kikazi ya siku saba ya kuimarisha uhai wa chama hicho mkoani Njombe. Kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Ludewa, Deo Filikunjombe na Mbunge wa Mwibara, Kange Lugora.
 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akimsadia Agnes Haule kutwanga mhogo alipomkuta akitwanga katika Kijiji cha Lupingu, Ludewa leo.
 Kikundi la ngoma ya mganda kikitumbuiza  wakati wa mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana katika Kijiji cha Lupingu, mwambao wa Ziwa Nyasa, Ludewa.
 Mbunge wa Mwibara, mkoani Mara, Kange Lugora akiungana na Consolata Kayombo kucheza noma ya Chioda wakati wa mkutano huo.
 Wananchi wa Lupingu, mwambao wa Ziwa Nyasa wakimbeba Mbunge wa Jimbo hilo, Deo Filikunjmbe wakati wa mkutano huo.
 Wananchi wakila kiapo cha utii cha CCM wakati wa mkutano huo
Katibu Mkuu wa CCM, AKinana akijadiliana jambo na Mbunge wa Lu, Deo Filikunjombe baada ya kumaiziza kuhutubia mkutano wa hadhara

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!