Bwana Ahmad Mohammed na Sayed Mousaviwakiwa mahakamani kenya kabla ya kuhukumiwa kifungo cha maisha jela
Raia wawili wa Iran wamehukumiwa kifungo cha maisha katika mahakama moja ya Kenya kuhusiana na mashtaka ya ugaidi.
Raia hao ni Ahmad Mohammed na Sayed Mousavi
ambao walishtakiwa wiki iliyopita kwa kumiliki vilipuzi, ambavyo
inaaminika vilikuwa vitumiwe kwa kufanya mashambulizi.
"mwili unanisisimka nikifikiria hasara ambayo
ingesababishwa na shambulizi hilo la kigaidi," amesema jaji Kiarie
Waweru Kiarie wakati akitoa hukumu hiyo.
Hata hivyo, serikali ya Iran imekana kuhusika na mpango huo wa kuishambulia nchi ya Kenya.
0 comments:
Chapisha Maoni