JOSE MOURINHO.
Kocha wa sasa wa Real Madrid JOSE MOURINHO ameweka wazi kwamba jumatatu wiki ijayo ataweka saini rasmi ya kuifundisha timu yake ya zamani CHELSEA The Blues,mkataba ambao utamuwezesha kuingiza kitita cha paundi milioni 12 kwa mwaka
Mourinho ambaye almekubaliana kuingia mkataba na mmiliki wa klabu hiyo tajiri wa kirusi ROMAN ABRAHAMOVICH ataenda London jumapili baada ya kukamilisha mchezo wake wa mwisho kuiongoza Madrid dhidi ya OSASUNA.
Stevan Jovetic
Mtihani wa kwanza wa Mourinho utakuwa ni kuwadhidi kete ARSENAL katika vita ya kuwania saini ya mshambuliaji steal Jovetic wa klabu ya FIORENTINA mchezaji mwenye thamani ya paundi milioni 25baada ya kushindwa kuinasa saini ya mshambuliaji CAVAN ambaye ameelezwa kuwa na thamani ya juu zaidi. 
CHRISTIAN RONALDO
wakati Mourinho akiondoka Madrid mreno mwenzake ambaye kulikua na tetesi za kutua naye Chelsea sasa Madrid wasema wapo kwenye mchakato wa kumfanya mreno huyo CHRISTIAN RONALDO kuwa mchezaji anayelipwa hela nyingi zaidi duniani ili kuhakikisha anabaki klabuni hapo ili kuzima ndoto za chelsea na manchester United kunasa saini ya nguli huyo wa soka duniani.
"Aliniambia kwamba hana raha ndani ya klabu na nikamuambia asijali,tutafanya kila njia kuhakikisha anakua na amani na raha ndani ya klabu kwasababu kwetu ni mchezaji bora duniani" alisema Perez.
THIAGO ALCANTARA
Mchezaji kiungo wa Barcelona akanusha uvumi kwamba ana mpango wa kusaini manchester United kufuatia ukimya wa Barcelona kuhusu mkata wake mpya.
FILLIPE MELO
wakala wa mchezaji Filipe Melo bwana Jose Rodrigo Baster amesema Manchester City wapo tayari kutoa kitita cha milioni kadhaa ili kuipata saini na huduma ya beki kisiki wa galatasarai ya uturuki mbrazili FILLIPE MELO
CHRISTIAN ERICKSEN.
Manchester United na Liverpool wapo vitani na Borussia Dortmund kuwania saini ya mchezaji wa Ajax CHRISTIAN ERICKSEN.
CLAUDIO RANIERI
Kocha wa zamani wa chelsea the blues Claudio Ranieri ametangazwa rasmi hii leo kuwa kocha mpya wa klabu ya MONACO na kumaliza uvumi kwamba Ranieri angetua West
Brom.
Muitaliano huyo amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu hiyo ya ufaransa
0 comments:
Chapisha Maoni