Searching...
Ijumaa, 17 Mei 2013

!!!CHUKUA TAHADHARI KUANGALIA HII!!!MAUAJI YA KUTISHA DAR ES SALAAM,MAJAMBAZI YAMCHINJA MLINZI NA KUMKATISHA KICHWA NA KIWILIWILI KAMA KUKU

Mlinzi wa baa ya Darajani Stop Over iliyo kando kando ya barabara kuu ya Morogoro Dar es salaam jirani na daraja la Mzambarauni  Bw Mika Athumani  amechinjwa na majambazi usiku wa kuamkia leo.Habari zilizoptaikana eneo la tukio zilidai kwamba majambazi  hao baada ya kuvamia baa hiyo iliyojitenga usiku wa manane  na kumvamia mlinzi huyo na kumchinja kama kuku na baadae kuvunja baa hiyo na kuimba vitu mbali mbali.
  Mwili wa marehemu ukiwa ndani ya gari, la polisi kufuatia mwili huo kutenganiswa vibande viwili..
Sehemu aliyochinjiwa mlinzi huyo aliyefahamika kwa jina la Mika Athumani.
Akihojiwa na blog hii mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi alidai kwamba majambazi hao walimvamia mlinzi wake na kumchinja na baadae walivunja Counter ya baa hiyo pamoja na duka lililopo jirani na baa hiyo na kuiba vitu mbali mbali.Alipoulizwa kwamba kuna taarifa zinadai kwamba mlinzi huyo alikutwa akiwa amelala Bw Mushi alisema inawezekana lakini hakuna mtu mwenye uhakika na jambo hilo kwani sote hatukuwepo,wakati tukio hilo linatokea"alisema Bw Mushi ambaye anadai bado hajafahami dhamani ya vitu vilivyoibikiwa na majambazi hayo.
Mwananachi akishuhudia damu ya mlinzi huyo kwa hudhuni
Baskeli ya Mlinzi huyo ikiwa imetapakaa damu ambapo inadaiwa mlinzi huyo alikuwa amelala kwenye eneo hilo
Redio ambayo majambazi hayo waliiangusha nje ya baa hiyo 
Majira ya saa 12 asubuhi ya leo wananchi walishuhudia maduka mawili ya baa hiyo yakiwa wazi huku mwili wa mlinzi huyo umekutwa upande wa baa ukiwa umechinjwa na kutenganishwa kichwa na mwili
Umati wa watu ukishuhudia tukio hilo muda mfupi uliopita.
Gari la polisi likiondoka eneo la tukio na mwili wa marehemu
Wananchi nao waliondoka eneo hilo la tukio.
Mmiliki wa baa hiyo Bw Salvatory Mushi akihojiwa na waandishi wa habari eneo la tukio.
            Majirani wa eneo hilo wakihojiwa na waandishi wa habari
                           Baadhi ya watu waliokuwepo eneo hilo la tukio walidai kwamba mlinzi huyo alikuwa amelala hivyo majambazi hayo yalimvamia na kumpora silaha zake na kisha kumchinja shingoni," siumeona alikuwa amelala jirani na baiskeli yake ndio maana ameshindwa kupambana nao hasa ukizingatia baa hii imejitenga iko peke yake hapa jirani na mto wa Morogoro"alisema Bw Maneo Mashani.
Mtandao huu ulishuhudia mtoto wa marehemu pamoja na mjukuu wa marehemu wakiangua vilio eneo la tuko baada ya kuuona mwili wa marehemu aliyeuwawa kikatili baadae wote wawili walipanda gari la polisi na kuondoka nao.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!