|
Mkuu
wa mkoa wa Singida, Dk.Parseko Kone(katikati) akifungua mkutano wa
maelewano katia ya kampuni ya JEO na Wind East Africa, zinazotarajiwa
kuzalisha umeme wa upepo katika manispaa ya Singida, viongozi wa
NDC,Tanesco makao makuu na viongozi wa ofisi ya mkuu wa mkoa
Singida.Naibu waziri wa nishati na madini Mh. George Simbachewene (wa
kwanza kushoto) ndiye aliyeitisha mkutano huo.Wa kwanza kulia ni Mkuu wa
wilaya ya Singida, Mwl.Queen Mlozi.
Mkurugenzi
wa kampuni ya Wind East Africa, Rashidi Shamte akitoa nasaha zake
kwenye mkutano huo wa maelewano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa
ofisi ya mkuu wa mkoa wa Singida.
Afisa
mwanadamizi wa shirika la Tanesco ambaye jina lake halikuweza
kupatikana mara moja akitoa nasaha zake kwenye mkutano wa maelewano wa
kampuni ya JEO na Wind East Africa.
Baadhi
ya maafisa waandamizi wa kampuni ya Wind East Africa wakifuatilia kwa
makini mkutano wa maelewano kati yao na wale wa JEO.
Baadhi
wa viongozi wa shirika la Tanesco wakifuatilia kwa makini mazungumzo
yaliyohusu maelewano kati ya kampuni ya Wind East Africa na JEO
yanayotarajiwa kuanza kuzalisha umeme wa upepo katika manispaa ya
Singida.
Naibu
waziri wa nishati na madini Mh. George Simbachawene akihutubia wakazi
wa kijiji cha Januka manispaa ya Singida.Mh. Simbachewene alifanya ziara
katika kijiji hicho kukagua maendeleo ya mradi wa kufua umeme wa upepo.
Baadhi
ya wananchi wa kijiji cha Januka manispaa ya Singida wakifuatilia kwa
makini hotuba iliyokuwa ikitolewa na naibu waziri wa nishati na madini
Mh. George Simbachawene (hayupo kwenye picha).Mkutano huo uliofanyika
kijijini hapo kwa ajili ya kuzungumzia mradi wa kufua umeme wa upepo
kijijini hapo.
(Picha zote na Nathaniel Limu).
|
Jumapili, 21 Aprili 2013
Related Posts
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
0 comments:
Chapisha Maoni