Searching...
Ijumaa, 5 Aprili 2013

KOREA YA KASKAZINI YAENDELEZA VITISHO VYAKE DHIDI YA MAREKANI

Korea Kaskazini imehamisha makombora mengine kwenye mwambao wake wa Mashariki tayari kwa mashambulizi dhidi ya Marekani, huku nchi hiyo inayotishiwa kushambuliwa ikisema inachukua tahadhari kubwa kutokana na vitisho hivyo.
Kulingana na chombo cha habari cha Yonhap cha Korea Kaskazini kikimnukuu afisa mmoja wa serikali nchini humo, kimesema makombora mawili tayari yameshasafirishwa kwa treni mapema wiki hii na kuwekwa katika magari tayari kwa kushambulia.
Kwa upande wake Wizara ya ulinzi ambayo ilithibitisha kupelekwa kwa kombora la kwanza ilikataa kutoa maoni yake juu ya habari za hivi karibuni kwamba makombora mengine yamesafirishwa Mashariki mwa pwani ya nchi hiyo.

 Rais wa Korea kaskazini Kim Jong Un akiwa pamoja na maafisa wake wa jeshi
Hata hivyo afisa mmoja wa jeshi amekiambia chombo hicho cha Yonhap kwamba, makombora yaliyosafirishwa yametegeshwa Mashariki na Magharibi mwa pwani ya Korea Kaskazini.
Vitisho hivyo vya Korea kaskazini ni mojawapo ya misururu ya vitisho vya wiki kadhaa sasa, kufuatia vikwazo vya Umoja Wa Mataifa dhidi yake na mazoezi ya pamoja ya kijeshi kati ya Marekani na Korea kusini.
Habari hii kwa hisani ya DW Swahili

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!