WAZIRI WA AFYA MH.DR.HUSSEIN MWINYI
IMEELEZWA kwamba inakadriwa kuwa asilimia saba ya idadi ya watu wazima wanaugua ugonjwa wa kisukari, lakini chini ya 1/3 ndio wanaofahamu wana tatizo hilo.
Kauli
hiyo imetolewa leo na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein
Mwinyi (Pichani) wakati akizindua kliniki ya vikoba ya wagonjwa wa
kisukari uliofanyika kwenye viwanja vya Mnazi mmoja jijini Dares Salaam.
Dk.
Mwinyi alisema watu wanaokabiliwa na tatizo hilo, wanafika hospitalini
wakiwa wameathirika figo, macho, shinikizo la damu au kukatwa miguu.
“
Ninaishauri jamii kutumia huduma hiyo ili kuweza kuchunguza afya zao na
kujinga kwa kufuata kanuni za afya kama vile kula vyakula visivyo na
mafuta mengi, sukari nyingi, chumvi kiasi, kula mboga za majani kwa
wingi na matunda,” alisisitiza. Dk. Mwinyi.
Aliongeza
pia jamii inatakiwa kufanya mazoezi ya kutosha, kupunguza uzito kwa
kiwango kinachotakiwa, kutovuta sigara na kupunguza kunywa pombe au
kuacha kabisa.
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
0 comments:
Chapisha Maoni