Searching...
Jumapili, 6 Aprili 2014

KATIBU MKUU WA CCM,KINANA AKAGUA MIRADI YA MAJI TAKA NA MAJISAFI WILAYANI SUMBAWANGA MKOANI RUKWA



Mkurugenzi wa Majisafi na Majitaka Sumbawanga (SUWASA), mkoani Rukwa, Antipas Shirima akitoa maelezo kwa Katibu Mkuu wa CCM, Ndugu Abdulrahman Kinana kuhusu ujenzi wa tanki la lita milioni moja za majisafi linalojengwa katika mradi wa SUWASA unaotarajiwa kumalizika Machi 7, mwakani (2015). Mradi huo mpaka unakamilika utagharimu kiasi cha fedha shilingi Bilioni 30.Pamooja na kutembelea mradii wa maji safi,Kinana pia alitembelea mradi wa maji taka wilayani humo mapema leo.Ndugu Kinana anamaliza zaira yake leo ya siku sita mkoani Rukwa.
Sehemu ya eneo hilo ambapo litajengwa tanki la lita milioni moja za maji safi na kusambazwa Wilaya ya sumbawanga na vijiji mbalimbali mkoani Rukwa.
Mkurugenzi wa Majisafi na Majitaka Sumbawanga (SUWASA), mkoani Rukwa, Antipas Shirima akimuelekea jambo Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kuhusu ujenzi wa eneo la kisima cha kuchujia maji safi na hatimaye kuyapeleka kwenye matanki na baadaye kusambazwa sehemu mbalimbali  za wananchi mkoani Rukwa.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!