WAHAMIAJI
haramu 100 raia wa Ethiopia wanashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani
Pwani kwa tuhuma ya kukutwa wameingia nchini bila kibali huku wakijua kuwa
kufanya hivyo ni makosa kisheria.
Raia
hao wamekamatwa ndani ya siku mbili mfululizo katika maeneo tofauti
ambapo kati yao Waethiopia 33 wao wametiwa mbaroni Februari 16 huko
kijiji cha Mwidu tarafa ya Chalinze wilayani Bagamoyo na 67 wamebambwa
februari 18 eneo la Mlandizi Kibaha.
Kaimu
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Mrakibu Msaidizi mwandamizi (SSP)
Athumani Mwambalaswa amethibitisha kukamatwa wahamiaji hao ambapo
amesema wote wamekamatwa majira ya saa nne asubuhi katika maeneo hayo
wakati askari polisi wakiwa doria.
Kamanda
Mwambalaswa amesema raia 33 waliokamatwa huko kijiji cha Mwidu wao
walikutwa wakiwa wamejificha katika msitu wa Magereza wakati askari
wakifanya ukaguzi maeneo hayo .
Ameongeza
kuwa katika tukio la pili waethiopia 67 nao wamekamatwa wakiwa
wamepakiwa kwenye gari T 943 BET aina ya Fusso lililokuwa likiendeshwa
na Ezekia Samson (31) huko Vikuruti Kibaha katika barabara kuu ya
Bagamoyo –Mlandizi.
Kaimu
kamanda huyo amesema kwa sasa wanaendelea kufanya mahojiano na
wahamiaji hao na kisha watawakabidhi idara husika ya Uhamiaji kwa hatua
zingine za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma
inayowakabili.

0 comments:
Chapisha Maoni