Searching...
Jumatano, 26 Februari 2014

MADIWANI WA CHADEMA WALIOJIUZULU WAJIUNGA RASMI NA CCM LEO

Mstahiki meya wa manispaa ya Shinyanga mheshimiwa Gulam Hafiz Mukadam akishikana mkono na aliyekuwa diwani wa kata ya Ngokolo katika manispaa ya Shinyanga bwana Sebastian Peter Mzuka maarufu kama Obama wa Ngokolo muda mucha baada ya kuwasili katika viwanja vya mahakama ya Mwanzo mjini Shinyanga katika mkutano wa katibu wa siasa na uenezi wa ccm taifa Nape Nnauye mkutano ambao wananchi wameouona kama ulikuwa na nia ya kuwapokea viongozi wa chadema Sebastiani Peter na Zacharia Mfuko wa kata ya Masekelo ambao kwa pamoja jana walifanya maamuzi ya kujivua udiwani wa kupitia tiketi ya CHADEMA. 
Waliokuwa madiwani wa CHADEMA,kulia ni Sebastian Peter,aliyekuwa diwani wa Ngokolo katikati ni Nape Nnauye na kulia ni Zacharia Mfuko aliyekuwa diwani wa Chadema kata ya Masekelo wakiwa juu ya jukwaa kabla ya kuvua magwanda na kurudisha kadi zao na kujiunga na CCM mbele ya Nape Nnauye jioni ya leo mjini Shinyanga
Mapema wakati wa mkutano wa hadhara wa Chama cha mapinduzi CCM jioni ya leo,Katibu wa siasa na uenezi CCM taifa Nape Nnauye akizungumza katika mkutano wa hadhara mjini Shinyanga katika viwanja vya mahakama ya mwanzo eneo la Nguzo Nane mjini Shinyanga.Kushoto ni mbunge wa jimbo la Shinyanga mjini,ambaye pia ni naibu waziri wa madini Stephen Masele.
Aliyekuwa diwani wa Chadema Zacharia Mfuko juu ya jukwaa la CCM kama unavyoona amevaa mali za CCM
Aliyekuwa diwani wa Chadema katika kata ya Ngokolo Sebastian Peter akizungumza katika mkutano wa CCM leo ambapo alisema ameamua kujiunga/kurudi nyumbani kwa hiari yake bila kushinikizwa na mtu yeyote na kukanusha habari zilizotapakaa mtaani kuwa yeye pamoja na mwenzake Zacharia Mfuko wamehongwa shilingi milioni 15 ili wahamie CCM
Nguo za CHADEMA walizokuwa wamevaa Madiwani hao walizokuja nazo mkutanoni walivua na kuamua kuchoma moto
Ndani ya gari la CCM Sebastian Peter na Zacharia Mfuko wakiondoka eneo la mkutano wameshavaa nguo za CCM kama unavyoona
Wanachama hao wapya wa CCM,Ndiyo gari waliyoondoka nayo eneo la mkutano
uh1
Kutoka kushoto ni Zakaria Martin Mfuko aliyekuwa Diwani wa Kata ya Masekelo(Chadema),na Kulia ni Sebastian Peter aliyekuwa diwani kata ya Ingokole(Chadema) wakitambulishwa mbele ya umati wa watu na Katibu wa NEC itikadi na uenezi Nape Nnauye kwenye viwanja vya Mahakama ya mwanzo Shinyanga mjini ambao kwa moyo mmoja wamejiunga na CCM.
uh2

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!