Miili hiyo ni ya watu wawili ambao walisadikiwa kuwa vibaka waliuwawa na
wananchi wenye hasira kali na kuchomwa moto na kisha kuzikwa katika makaburi yaliyopo katika kijiji
hicho.
Kwa mujibu wa mashuhuda
wakizungumza mwandishi wetu
wamesema hali hiyo imetokana na kuzikwa
katika makaburi ambayo hayana kina kirefu hivyo wanyama hao kuwa rahisi
kwao kufukua na kuanza kula maiti hizo....
Mmoja wa mashuhuda Hasan
Msoma amesema waligundua kutokana na wao
kufika katika maeneo ya makaburi kwa lengo la kuzika Mtoto ndipo wakaona mabaki
ya miili ya marehemu huku eneo kubwa la miili ikiwa imeliwa na fisi.
Amesema baada ya kuona hali hiyo waliutaarifu uongozi
wa kata ambao ulifika na kushiriki katika
mazishi na kusema kuwa haki za
binadamu hazikuzingatiwa katika kuzika
watu hao kwani walifukiwa katika shimu lenye kina kifupi cha futi moja.
Hata hivyo viongozi wa kata
hiyo hawakuwa tayari kuzungumzia suala hilo kutokana na kutoonesha ushirikiano kwa mwandishi wetu.
0 comments:
Chapisha Maoni