Searching...
Ijumaa, 3 Januari 2014

SHERIA YA MLINDA ZITO,MAHAKAMA YAZUIA CHAMA KUMJADILI LEO KIKAONI.

          Zitto Kabwe akiingia mahakama Kuu Dar es Salaam jana.
 Wanasheria wa Chadema, Tundu Lisu (kushoto) na Peter Kibatala waliofika kupinga hoja hiyo mahakamani.
 Tundu Lisu na Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema wakijadiliana jambo wakati wakisubiri uamuzi wa mahakama
Zitto na wakili wake Msando wakiwasiliana na marafiki zao walipokuwa wakisubili uamuzi wa mahakama, ambapo Zitto aliibuka kidedea kwa pingamizi lake kukubaliwa hivyo kikao cha Kamati Kuu ya CHADEMA iliyokuwa imepangwa kufanyika leo kukatazwa kumjadili Zitto kwa namna yoyote ile.

 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe (kulia) akitoka katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Dar es Salaam, ambapo aliwasilisha ombi la pingamizi la yeye kujadiliwa kwenye kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kinachotarajia kufanyika leo, hadi rufaa yake ya kupinga kuenguliwa wadhifa huo kwenye Baraza Kuu la chama hicho. Kushoto ni Wakili wa Zitto, Albert Msando. Mahakama Kuu imekubaliana na Zitto Kikao cha Kamati Kuu ya Chadema kinachotarajiwa kufanyika leo kutomjadili kwa namna yoyote ile.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!