
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo
ya Vijana Mheshimiwa Makongoro Mahanga.
Baadhi ya nakala za malada ya kesi hiyo
iliyofunguliwa mahakama ya kazi, Tume ya Usuluhishi na Upatanishi na
Bi. Itika Kasambala dhidi ya Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo
ya Vijana.
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,
Dkt Mahongoro Mahanga akitoka katika chumba cha mahakama ya kazi, Tume
ya Usuluhishi na Upatanishi wiki iliyopita siku ya Jumanne baada ya
kusomewa mashtaka yake ya kumfanyisha kazi PS wake (Private Secretary)
Bi, Itika Kasambala katika ofisi yake ya Bunge kwa muda wa miaka kumi
bila mkataba na kusitisha kazi yake na kisha kulipa mafao ya laki mbili
tu
Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana
akishuka katika kazi za mahakama ya kazi, Tume ya Usuluhishi na Upatanishi
wiki iliyopita siku ya Jumanne jijini Dar es Salaam.
Bi. Itika Kasambala akiwa katika moja ya vyumba vya
habari baada ya kufanya mahojiano na mwandishi wa habari hizi
Bi Itika kasambala akiwa katika picha tofauti jijini
Dar es Salaam baada ya kuelezea sakata lake na Naibu Waziri wa kazi,
Ajira na Maendeleo ya Vijana
----
Na. Mwandishi wetu
NAIBU Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,
Dkt Makongoro Mahanga ameingia kwenye kashfa nzito ya kuvunja sheria
za kazi nchini kwa kumfanyisha kazi msaidizi wake (PS) wa ofisi yake
ya Bunge kwa miaka kumi bila mkataba na kumlipa fedha taslimu shilingi
laki mbili tu (200,000) kama mafao.
Naibu Waziri, Mahanga anakuwa kiongozi wa kwanza kuingia
kwenye kashfa akiwa madarakani tena kwenye swala la ajira wakati yeye
mwenyewe ni waziri mwenye dhamana na maswala ya ajira na haki za wafanyakazi
nchini chanzo chetu kimeelezwa.
Kwa mujibu wa sheria za kazi na mahusiano kazini, Naibu
Waziri amekiuka kifungu cha 3 cha sheria ya Taasisi za kazi za mwaka
2004 na pia amekiuka sehemu ya tatu ya viwango vya ajira na sehemu ndogo
A kwa kushidwa kuandika mkataba kwa mujibu wa kifungu cha 14 ibara ya
kwanza kama sheria ya kazi na mahusiano kazini inavyotaka.
0 comments:
Chapisha Maoni