Searching...
Jumapili, 5 Januari 2014

MAKAMU WA RAIS ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA KIFO CHA DR.WILLIAM MGIMWA

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisani Kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dkt. William Mgimwa, aliyefariki dunia Januari 01, 2014 huko nchini Afrika Kusini alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Dr. Bilal alipofika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, leo jioni. Picha na OMR
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mke wa marehemu Dr. Mgimwa, Jane Mgimwa, wakati alipofika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, leo jioni.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji wanafamilia wa marehemu Dr. Mgimwa, wakati alipofika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, leo jioni.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete, akisaini Kitabu cha maombolezo ya kifo cha aliyekuwa Waziri wa Fedha, Dkt. William Mgimwa, aliyefariki dunia Januari 01, 2014 huko nchini Afrika Kusini alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Dkt. Bilal alifika kuhani msiba huo nyumbani kwa marehemu Mikocheni B, jijini Dar es Salaam, 04.01.2014. Picha na OMR

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!