Searching...
Jumatano, 4 Desemba 2013

KILIMANJARO STARS YAICHAPA BURUNDI,YATINGA ROBO FAINALI,SASA KUIVAA UGANDA THE CRAINES

 
Timu ya soka ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars leo jioni imeitandika timu ya taifa ya Burundi bao moja kwa bila na kutinga hatua ya robo fainali.
 
Kilimanjaro Stars sasa itamenyana na Uganda, The Cranes katika Robo Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge, Desemba 7, mwaka huu Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya.
Hiyo inafuatia Zambia kuifunga Somalia mabao 4-0 katika mchezo wa pili wa Kundi B jioni hii Uwanja wa Afraha, Nakuru, Kenya, huo ukiwa ushindi mkubwa zaidi katika mashindano hayo hadi sasa.
Mabao ya Zambia yamefungwa na Bornwell Mwape na Festus Mbewe, kila mmoja mawili.
Katika mchezo uliotangulia, bao pekee la Mbwana Ally Samatta kwa kichwa dakika ya saba tu ya mchezo huo, akiunganisha krosi maridadi ya mshambuliaji mwenzake wa TP Mazembe ya DRC, Thomas Ulimwengu liliipa Stars ushindi wa 1-0 dhidi ya Burundi.
Ikumbukwe mara ya mwisho Stars ilipokutana na The Cranes yenye wachezaji nyota kama Emmanuel Okwi aliyewahi kuchezea Simba na Hamisi Kiiza anayechezea Yanga za Dar es Salaam, ilifungwa mabao 3-0 mwaka jana katika Nusu Fainali mjini Kampala, Uganda.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!