Searching...
Jumamosi, 2 Novemba 2013

DUNIA IMEKWISHA: MWANAFUNZI AUAWA KWA KUTUHUMIWA KUIBA MAANDAZI JIJINI MBEYA

MWANAFUNZI mmoja ameuawa kwa kipigo na mwili wake kutupwa kichakani akituhumiwa kuiba maandazi. Mwanafunzi huyo (jina limehifadhiwa) alikuwa akisoma darasa la pili katika Shule ya Msingi Nyakadete, iliyopo wilayani Mbarali mkoani Mbeya.
 
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Robert Mayala, alidai kuwa mwanafunzi huyo mkazi wa Kijiji cha Nyanyembe Kata ya Madibira, aliuawa kwa kupigwa na kisha mwili wake kutupwa vichakani akituhumiwa kuiba maandazi.
 
 
Kamanda Mayala alidai mwili wa mwanafunzi huyo ulikutwa Jumatatu saa 4:00 asubuhi, ukiwa kichakani katika Kijiji cha Unyanyembe Nyamakuyu Kata ya Madibira.
 
Kutokana na tukio hilo, polisi wanamshikilia Edmund Kwinge (30) mkazi wa Kijiji cha Nyakadete, akituhumiwa kuhusika na mauaji ya mwanafunzi huyo na atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi kukamilika.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!