Searching...
Jumanne, 15 Oktoba 2013

BALAA KUBWA MADRID,WAMELIWA KUMSAJILI BALE-DAKTARI.

Madrid up Bale bid after Coentrao snub  
GARETH BALE.
Agosti mwaka huu, Real Madrid, ilifanya kufuru baada ya kuvunja benki na kuandika historia mpya kwenye soka kwa kufanya usajili wa pesa nyingi zaidi duniani. Ni wakati walipomnasa winga wa Wales, Gareth Bale, kwa uhamisho wa Pauni 85 milioni.
Uhamisho ulikuwa gumzo Ulaya nzima na kuwafanya watu wengine wafike mbali na kuchambua mambo mengine ambayo yangeweza kufanywa kwa kutumia pesa hiyo ya usajili wa Bale.
Lakini hata mwaka ukiwa haujaisha, tayari Real Madrid inaonekana kama imeingia mkenge kwenye usajili huo uliowagharimu pesa nyingi.
Daktari asema Real Madrid imeliwa
Katika kusaka ukweli wa kitaalamu kuhusiana na maradhi ya mgongo yanayomsumbua Bale, gazeti maarufu jijini Madrid, MARCA lilifanya mahojiano na madaktari mbalimbali mahiri wa Kihispaniola.
Wakamfuata daktari mwenye hadhi kubwa, Avelino Parajon na akasema hivi: “Kama Real Madrid ilimsajili Gareth Bale ikidhani kwamba hili ni tatizo dogo tu, wamefanya kosa kubwa sana.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!