Searching...
Alhamisi, 12 Septemba 2013

WAZIRI DK. EMMANUEL NCHIMBI AZUNGUMZA NA WATUMISHI WA IDARA YA UHAMIAJI MAKAO MAKUU NA MKOA WA DAR ES SALAAM LEO.



 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na watumishi wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu pamoja na wawakilishi wa idara hiyo Mkoa wa Dar es Salaam (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya utendaji kazi wa idara hiyo. Kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil pamoja na Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile Mwakinyule. Dk Nchimbi aliwataka watumishi hao kufanya kazi kwa uadilifu. Mkutano huo ulifanyika katika ofisi za Uhamiaji Makao Makuu, jijini Dar es Salaam leo. (Picha na Felix Mwagara, Wizara Mambo ya Ndani ya Nchi).
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na watumishi wa Idara ya Uhamiaji Makao Makuu pamoja na wawakilishi wa idara hiyo Mkoa wa Dar es Salaam. Dk Nchimbi alifanya ziara ya siku moja katika Ofisi za Makao Makuu ya Idara hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam leo kwa lengo la kuzungumza na watumishi hao masuala mbalimbali ya utendaji kazi.. (Picha na Felix Mwagara, Wizara Mambo ya Ndani ya Nchi).
 Kamishna wa Pasipoti na Uraia, wa Idara ya Uhamiaji, Victoria Lembeli (kushoto) akimuuliza swali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (wa pili kutoka kulia) kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya idara hiyo. Watumishi mbalimbali waliuliza maswali pamoja na kutoa maoni yao katika mkutano huo uliofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya idara hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Naibu Waziri wa wizara hiyo, Pereira Ame Silima. Kushoto (Meza Kuu) ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mbarak Abdulwakil pamoja na Kamishna Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Sylvester Ambokile Mwakinyule. (Picha na Felix Mwagara, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.).

0 comments:

Chapisha Maoni

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Back to top!