Searching...
Jumamosi, 21 Septemba 2013

SERENGETI FIESTA MUSOMA,ILIKUA NI BALAAA...ANGALIA MWENYEWE

Mwanadada Shilole akionesha umahiri wake wa kunengua jukwaani mbele ya maelfu ya watazamaji waliojitokeza usiku wa jana kwenye tamasha la Serengeti fiesta 2013.
 Anaitwa Linah Sanga,kutoka nyumba ya vipaji THT akiimba jukwaani usiku huu
 Watu kibao,kila mmoja akijiachia kivyake huku jukwaa likiwaka moto vilivyo kwa miondoko ya bandika bandua ya wasanii wanaotumbuiza. 
 Wakali wengine wanaokuja kwa kasi katika anga la bongofleva-hip hop,Stamina na Youngkiller wakilishambulia jukwaa kwa kushusha mistari mikavu live.
 Shangwe kila kona za mashabiki zimetawala uwanjani hapa.
 Msanii wa muziki wa bongofleva ambaye kwa sasa anafanya vyema kwenye anga hizo,Neylee akiimba jukwaani usiku wa jana wakati wa tamasha la serengeti fiesta 2013 likiendelea usiku huu ndani ya uwanja wa Karume,Musoma mkoani Mara.
 Kundi la Wanaume TMK Halisi likiongozwa na msanii nguli Juna Nature wakilishambulia vyema jukwaa usiku huu kwa staili yao mapanga shaa shaa,huku mayowe yakipigwa kutoka mashabiki.
Kila shabiki alikuwa na mzuka wake.
 Mashabiki wa tamasha la serengeti fiesta wakifuatilia yanayojiri ndani ya uwanja wa Karume hivi sasa.

0 comments:

Chapisha Maoni

:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Back to top!