Searching...
Alhamisi, 1 Agosti 2013

MKUU WA MKOA WA RUKWA AZINDUA UZIO ULIOJENGWA KWA FEDHA ZA WAHISANI KUTOKA MAREKANI KATIKA KITUO CHA WATOTO YATIMA CHA ST. MARTIN DE PORES KATANDALA MKOANI RUKWA

Baba Askofu Kiharuzi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga katikati akibariki tukio hilo. Geti linaloonekana ni sehem ya uzio wa huo uliojengwa kwa fedha za wahisani kutoka Marekani. Katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliendesha harambee fupi ya kuchangia kituo hicho ambapo jumla ya Tsh. 835, 000/ zilipatikana.  
  Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikabidhi zawadi ya batiki kwa Mama Ann Marie English pamoja na wahisani wengine sita kutoka Marekani ambao ni mmoja kati ya wahisani waliofadhili miradi hiyo mbalimbali katika kituo hicho cha St. Martin De Pores.  
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikabidhi Hati ya Pongezi kwa Mama Ann Marie English pamoja na wahisani wengine sita kutoka Marekani ambao ni mmoja kati ya wahisani waliofadhili miradi hiyo mbalimbali katika kituo hicho cha St. Martin De Pores.
 Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya akikabidhi zawadi ya nembo ya bendera ya Taifa kwa Mwenyekiti wa jumuiya ya St. Martin Kids ya Marekani Mama Marry Lynne Cassleman na wahisani wengine sita kama kumbukumbu kwako kwa kufika Mkoani Rukwa.
Mwenyekiti wa jumuiya ya St. Martin Kids ya Marekani Mama Marry Lynne Cassleman akizungumza katika hafla hiyo.
Ndugu Michael Caraway ambaye ni mmoja ya wahisani hao kutoka Marekani akizungumza katika hafla hiyo. Kulia anaeonekana kichwa kwa nyuma ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhandisi Stella Manyanya.
 Ndugu Michael Caraway kulia aliomba kupiga picha ya kumbukumbu na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.
Picha ya pamoja
Na
 Hamza Temba 
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!