Searching...
Alhamisi, 11 Julai 2013

MANCHESTER CITY KUISTUA DUNIA-KUMSAJILI CHRISTIAN RONALDO.



manchester city, cristiano ronaldo, manchester united, transfer Klabu ya Manchester City wapo mbioni kuvunja benk ili kunyakua mshambuliaji wa Real Madrid Mreno aliyekua akikipiga zamani na klabu ya Manchester United Cristiano Ronaldo



Man City wameamua kuvunja Bank ili kutoa kitita kikubwa ambacho kitaweza kuwashawishi Real Madrid pamoja na Ronaldo mwenyewe kutua  Etihad msimu ujao wa ligi kuu England
Habari za neema zaidi kwa Ronaldo zinasema Man City wamemuambia wakala wa Ronaldo kwamba wapo tayari wamejiandaa kumlipa kiasi chochote cha fedha zaidi ya kile alichoahidiwa na Man U kwa maana kwamba wanaweza kumlipa zaidi ya paundi laki tatu kwa wiki 
United have spent the past five months trying to put together a deal to bring Ronaldo back  
Manchester United wamejitahidi kwa takribani miezi mitano iliyopita kumrudisha mshambuliaji huyo bila mafanikio lakini wao City wameamua kuvunja bank ili kumvutia Ronaldo.



Mwenyekiti wa Man City Sheik Mansur ameweka wazi kwa Soriano kwamba klabu yake itafanya kila linalowezekana ikiwa ni pamoja na kutumia kitita chochote cha fedha kuinasa saini ya mreno huyo ambaye kiwango chake kinakua kila kukicha
Ronaldo bado ana mkataba wa miaka miwili na klabu ya Madrid


City's chief executive and football director have told Ronaldo's reps they are serious with their interest  
Mkurugenzi mtendaji na mkurugenzi wa ufundi wa Man City wamemuambia wakala wa Ronaldo kwamba wapo tayari kufanya lolote muda wowote,


Hata hivyo Paris Saint Germain ni timu pekee inayoweza kuweka mezani kitita kikubwa kama cha City japo tayari ofa yao ya kutoa paundi milioni 55 kumyakua Ronaldo ilikataliwa na Madrid wiki iliyopita


Former United boss Sir Alex Ferguson made Ronaldo a global superstar  
Kocha wa zamani wa Man U Sir Alex Ferguson ndiye aliyemuibua na kumfanya mchezaji bora duniani ambapo mpaka sasa United wapo tayari kurudisha paundi milioni 70 kwa Madrid ili kumrejesha Old Trafod lakini wakala wa Ronaldo amesema itakuwa ni vigumu sana kwa Madrid kukataa ofa ya Man City kwani ni kitita kikubwa sana.
Ronaldo spent six successful seasons at Old Trafford

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!