Jose Mourinho amekaririwa na mtandao wa klabu hiyo akisema yupo tayari kumsainisha Juan Mata mkataba mnono na mrefu wa miaka mitano
Taarifa zaidi zinasema huenda Demba Ba na Fernando Torres wakatimka klabuni hapo kwani hawapo kwenye orodha ya Mourinho
RAMIRES.
Mchezaji mwingine
anayetarajiwa kusalia klabuni hapo ni mbrazili kiungo Ramires baada ya
kuweka wazi kwamba Mourinho amempigia simu na kumjulisha kwamba
ataendelea kusalia klabuni hapo msimu ujao.
Ramires
ambaye ameondolewa na kocha wa brazil Luiz Felipe Scolari kwenye orodha
ya kikosi cha Brazil kinachoendelea na mashindano ya kombe la
confederations amesema kwa sasa anaendelea na mapumziko huko nyumbani
kwao Brazil.
“ninayo furaha kubwa sana kufanya kazii na Mourinho.
“ amenipigia siku chache zilizopita,kitu ambacho kilinishangaza na kunifurahisha sana
“ameniambia mambo mazuri mengi sana ikiwa ni pamoja na ukweli kwamba alijaribu kunisajili kwa kipindi chote akiwa Inter Milan na Real Madrid kipindi hicho nikiwa Benfica.
“Mourinho ameniambia anayofuraha kubwa sana kufanya kazi na mimi Chelsea...kwakweli ninayo furaha sana...Alisema Ramires.
0 comments:
Chapisha Maoni