Searching...
Jumatatu, 27 Mei 2013

TAHARUKI YA MABOMU MAKETE -MKOANI NJOMBE YAONGEZEKA

 
       RPC-NJOMBE
NA EDWIN MOSHI, MAKETE
Wakazi wa Makete mjini hasa waliokaribu na kituo cha polisi Makete wamekumbwa na taharuki na mshituko wa hapa na pale kufuatia milio ya mabomu iliyokuwa ikisikika tokea kituoni hapo

Hali hiyo iliyotokea leo hii imewashangaza wengi na kuwaacha na sintofahamu huku wengi wao wakidhani kuwa yale ya liyotokea Arusha yamebisha hodi Makete


Kutokana na taharuki hiyo, mtandao huu ulibisha hodi kituoni hapo na kukutana na Mkuu wa polisi wilaya ya Makete SP Peter Kaiza (Pichani)ambaye alilitolea ufafanuzi suala hilo na kusema kwamba hali hiyo imetokea kwa kuwa walikuwa wakifanya mazoezi ya kutuliza ghasia ama vurugu, ambapo iliwalazimu kulipua mabomu

“Huo ni utaratibu wa jeshi kutokana na kufanya mazoezi mbalimbali, mara ya mwisho tulilipua mabomu mwaka 2010 mwezi januari, tumekuwa tukiwa katika mazoezi tunafanya hivyo na hii pia inasaidia kuweka askari wetu tayari, na pia wananchi kufahamu kama hali hiyo ikitokea hali inakuwaje” alisema Kaiza

Akizungumzia kuhusu kutoa taarifa kwa wananchi, SP Kaiza amesema wangeweza kutoa taarifa kwa wananchi ingawa walitoa taarifa kwa uongozi wa wilaya, lakini wakati mwingine mabomu hulipuka eneo lolote bila taarifa na kwa kufanya hivyo kunasaidia kuwaweka tayari wananchi

Amesema mabomu hayo hayana madhara na hakuna tukio baya lililotokea, hivyo kuwataka wananchi kuondoa hofu na kuendelea na shughuli zao kama kawaida

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!