Searching...
Jumamosi, 4 Mei 2013

MEI MOSI SINGIDA ZAFANYIKA JANA UWANJA WA NAMFUA.

Wafanyakazi wa mkoa wa Singida na wananchi kwa ujumla, waungana na wenzao kuadhimisha siku ya wafanyakazi duniani (mei mosi) yaliyofanyika jana kimkoa kwenye uwanja wa michezo wa Namfua.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,akipokea maandamano ya wafanyakazi jana ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za siku ya wafanyakazi dunia zilizofanyika kwenye uwanja wa Namfua mjini Singida.
Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,jana akihutubia baadhi ya wafanyakazi na wananchi wa mkoa wa Singida waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (mei mosi) zilizofanyika kwenye uwanja wa Namfua.
 Mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone,jana akimkabidhi mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Manyoni,Fortunata Mallya cheti cha mfanyakazi bora baada ya mkurugenzi huyo kuchaguliwa kuwa mfanyakazi bora wa halmashauri ya Manyoni kwa mwaka wa 2013/2014.
Baadhi ya viongozi wa ngazi mbalimbali wa mkoa wa Singida,waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani (mei mosi) zilizofanyika jana kimkoa katika uwanja wa Namfua mjini Singida.
 
Kikundi cha uhamasishaji cha kata ya Kindani manispaa ya Singida kikitoa burudani kwenye maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani zilizofanyika kimkoa kwenye uwanja wa namfua mjini Singida.
Baadhi ya wafanyakazi wa sekta mbalimbali mkoani Singida,waliohudhuria maadhimisho ya sherehe za wafanyakazi duniani zilizofanyika kimkoa katika uwanja wa namfua mjini Singida.
(Picha zote na Nathaniel Limu).


0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!