Searching...
Jumanne, 21 Mei 2013

BREAKING NEWS: PROFESSOR JAY AJIUNGA NA CHADEMA/ AKABIDHIWA KADI YA UANACHAMA DODOMA

BKyYkGxCYAA-P5B.jpg_large
Pichani Professor Jay akiwa na Kiboya,mdau mkubwa wa muziki nchini ambaye pia ni mwanachama wa CHADEMA. Picha kwa hisani ya Twitter ya Professor.
Habari ambazo zinatambaa hivi sasa mtandaoni ni kwamba msanii maarufu na miongoni mwa wanaoaminika kuwa waasisi wa muziki wa Hip Hop nchini Tanzania, Professor Jay (jina halisi Joseph Haule), amejiunga rasmi na harakati za siasa nchini kwa kujiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Professor Jay ambaye tungo zake mara kwa mara zimekuwa zikijikita katika kutetea maslahi ya wananchi, amejiunga na CHADEMA huko Dodoma ambapo amekabidhiwa rasmi kadi ya uanachama.
Zoezi hilo limesimamiwa na John Mnyika, Mbunge wa Ubungo na Joseph Mbilinyi (Sugu) Mbunge wa Mbeya Mjini na kushuhudiwa na wanachama wengine kadhaa ambao aidha ni wanamuziki pia au wadau wa karibu wa muziki.
Bila shaka kujiunga kwa Professor Jay na CHADEMA kunaashiria kwamba yupo mbioni kugombea Ubunge katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015. Professor Jay ni mwenyeji wa Mikumi-Morogoro na hivyo haitoshangaza kama ataamua kugombea katika jimbo hilo hapo mwaka 2015.
Professor Jay ajiunga CHADEMA
Professor Jay akikabidhiwa kadi na Mh.Joseph Mbilinyi.


0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!