SIR ALEX FERGUSON
Karatasi iliyotumika kuorodhesha majina ya wachezaji kumi na moja wa timu ya MANCHESTER UNITED ikiwa ni mechi ya kwanza kwa kocha mstaafu SIR ALEX FERGUSON kuiongoza klabu hiyo tarehe 08.11.1986 sasa kupigwa mnada wiki hii.
mechi hiyo MAN U walikula kichapo cha magoli 2-0 kutoka kwa OXFORD UNITED
HII NDIYO KARATASI YENYEWE NA ORODHA KAMILI YA WACHEZAJI 11 ALIOWATUMIA SIR ALEX FERGUSON KATIKA MECHI YAKE YA KWANZA KUIONGOZA MAN UNITED TAREHE 08.11.1986
Timu hii ilikua imevaa T-Shirt Nyekundu,kaptula nyeupe na socks nyeusi kipindi hicho bado akina GIGGS na SCHOLES walikua bado hawajasajiliwa.
LUIS SUAREZ
mshambuliaji nguli wa liverpool Luis Suarez amesema itakua ni vigumu sana kukataa ofa ya kutua Real Madrid,Suarez alisaini mkataba mrefu mwaka jana kuitumikia Liverpool pamoja na kwamba aliifungia klabu hiyo magoli 30 msimu uliopita lakini anakabiliwa na adhabu ya kukaa benji mechi kumi baada ya kumng'ata beki wa chelseaBranislav Ivanovic
Vita ya kumgombea mchezaji nguli wa kabu ya Tottenham imezidi kufukuta na sasa imechukua sura mpya baada ya CHELSEA na MANCHESTER UNT kupanda dau la paundi milioni 80 tofauti na MADRID waliotaka kutoa paundi milioni 60 na kuifanya klabu hiyo sasa kuamini kwamba uwezekano wa kumbakisha BALE klabuni hapo haupo tena na badala yake ni kumuachia mchezaji mwenyewe aamue anatua klabu gani,japo habari za ndani za TOTTENHAM zinasema wao wasingependa kumuona Bale akihamia klabu ya England.
Vita vipya vimeanza kati ya mahasimu wawili MANCHESTER UNITED na MANCHESTER CITY kumgombea kiungo mshambuliaji wa Barcelona Cesc Fabregas ili kumrejesha katika ligi kuu England msimu ujao,Huku Arsenal wakiwa hawajui cha kufanya.
Huyu ndiye kocha mpya wa MANCHESTER UNITED David Moyes ambaye anamtaka CESC kutua Old Tranford msimu uja.
MANUEL PELLEGRIN
Huyu ndiye kocha mkuu mpya wa Manchester City ambaye naye pia anamuwania kiungo mshambuliaji CESC FABREGAS
0 comments:
Chapisha Maoni