Searching...
Ijumaa, 26 Aprili 2013

SAKATA LA SUAREZ LAINGIA IKULU...KAULI YA WAZIRI MKUU YALETA MALUMBANO MAKALI NA KLABU





 Luis Suarez, David Cameron
Waziri mkuu wa Uingereza bwana David Cameron amesema kitendo kilichofanywa na mshambuliaji wa Liverpool Luis Suarez kumng’ata bila huruma Branislav Ivanovich kimekua ni mfano mbaya sana katika soka la nchi hiyo..
"kama baba na binadamu wengine nafikiri tunapaswa kuweka adhabu kali sana wenye tabia kama hizi" alisema bwana Cameron.
Hata hivyo Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amelalamikia kauli ya kwanza aliyoitoa waziri mkuu huyo kwamba ilichangia kwa kiasi kikubwa mchezaji wake kupewa hukumu kubwa ya kufungiwa mechi kumi.
Kabla ya kamati kukaa ili kujadili adhabu hiyo bwana Cameron alikaririwa akisema kwamba ”itakua ni kitu kisichoeleweka endapo tu kamati hiyo itachukulia kwamba wachezaji maarufu siku zote ni watu wa kuigwa”kauli ambayo iliwafadhaisha na kuwastua Liverpool.
"Hii ni mara yangu ya kwanza kusikia kamati iliyo huru kuingiliwa na watu wengi na viongozi wa juu wa nchi..alisema Rogers."
Hata hivyo bwana Cameron alijibu mapigo ijumaa hii asubuhi na kumbwatukia bwana Rogers kwamba yeye yupo huru kutoa maoni yake pasipo kujali cheo chake.
"mimi nimeweka mawazo yangu sawa …mimi kama baba niliyekua nikiangalia mchezo ule bwana Cameron …mimi nina mtoto mwenye umri wa miaka saba ambaye ni mpenzi mkubwa wa mchezo wa mpira wa miguu,kwahiyo wakati wachezaji wanapokuwa na tabia kama hizi ni mfano mbaya sana kwa kizazi cha vijana wadogo wa taifa letu….alimalizia bwana Cameron

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!