Searching...
Jumatatu, 9 Desemba 2013

RATIBA KAMILI YA KOMBE LA FA YATOKA,NI VITA KATI YA ARSENAL Vs TOTTENHAM

Jubilant: Wigan won the FA Cup last season against all odds by beating Man City in the final
KLABU ya Arsenal imepangwa na wapinzani wao wa London Kaskazini, Tottenham katika Raundi ya Tatu yaKombe la FA.
Manchester City watasafiri kuifuata Blackburn Rovers, Chelsea watamenyana na Derby ugenini na Manchester United watakuwa wenyeji wa Swansea.
Mabingwa wa sasa, Wigan wataanza kampeni zao za kutetea taji kwa kumenyana na Milton Keynes Dons nyumbani.

Mechi kali; Arsenal itamenyana na Tottenham Uwanja wa Emirates 
Jubilant: Wigan won the FA Cup last season against all odds by beating Man City in the final
Wigan ilishinda Kombe la FA msimu uliopita baada ya kuifunga Man City katika fainali
Aidha, Liverpool itamenyana na Oldham au Mansfield Uwanja wa Anfield, wakati West Brom itacheza na Crystal Palace, Newcastle na Cardiff na Norwich na Fulham. 
Oldham iliifunga The Reds 3-2 katika Raundi ya Nne mara ya mwisho na watakutana na kikosi cha Brendan Rodgers kama wataitoa Mansfield katika mchezo wao wa marudiano wa Raundi ya Pili.
Liverpool pia ilikutana na Mansfield katika Raundi ya Tatu msimu uliopita, na Luis Suarez aliiongoza timu yake kushinda 2-1.
Tricky customer: Luis Suarez helped knock out Mansfield with a handball last season
Luis Suarez aliisaidia Liverpool kuitoa Mansfield 
Mara ya mwisho Arsenal kushinda Kombe la FA ilikuwa mwaka 2005, lakini ili kushinda taji hilo tena italazimika kuwafunga wapinzani wake wakuu.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!