Searching...
Jumatatu, 9 Desemba 2013

RAIS WA KENYA BW.UHURU KENYATTA AVUNJA SAFARI YA KUTEMBELEA KIBERA

 
 RAIS WA KENYA BWANA UHURU KENYATA.
Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amevunja ziara yake ya kushiriki kwenye hafla ya kuwakabidhi Wakenya wenye asili ya Kinubi hati za kumiliki vibanda vyao kwenye eneo la mabanda la Kibera la mjini Nairobi kwa sababu za kiusalama.  
WAZIRI WA ARDHI WA KENYA BI.CHARITY NGILU.
Vyombo vya habari vimeripoti kuwa, washauri wa Kenyatta wamemshauri asihudhurie hafla hiyo iliyoitishwa na Waziri wa Ardhi wa Kenya Bi Charity Ngilu kwa sababu jambo hilo limelalamikiwa na wakazi wa Kibera. Huku hayo yakiripotiwa, habari kutoka mjini Nairobi zinasema kuwa, hafla ya kukabidhi hati miliki iliyokuwa imepangwa kufanyika leo huko Kibera, imevunjwa.  
 
WAKAZI WA KIBERA NCHINI KENYA WAKATI WA UCHAGUZI ULIOPITA.
Baadhi ya wakazi wa eneo hilo wamelalamika kuwa wamedharauliwa katika suala hilo na wametishia kuvunja usalama wa eneo hilo.  
MSEMAJI WA RAIS WA KENYA BW.MANOAH ESIPUSU.
Hata hivyo msemaji wa Rais Kenyatta, Manoah Esipusu amesema kuwa Kenyatta hakuwa amepanga kushiriki kwenye hafla hiyo na wala ziara hiyo haikuwemo kwenye ratiba zake za leo.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!