Searching...
Jumatatu, 2 Septemba 2013

MAMA AOLEWA NA MWANAYE WA KUMZAA ,TAYARI NI MJAMZITO



 
Kichwa cha habari peke yake kinatisha,jaribu kufikiria kama hili linawezekana katika dunia hii??? amini usiamini bibie Betty Mbereko mwenye umri wa miaka 40 amefikia maamuzi ya kuolewa na mwanaye wa kumzaa mwenyewe,ambaye ni mtoto wa kwanza wa uzao wake.

Mtoto huyo aliyejulikana kwa jina la Farai Mbereko mwenye umri wa miaka 23 inasemekana amekua akiwa na mahusiano ya kimapenzi ya siri na mama yake miaka mitatu iliyopita mara tu baada ya baba yake kufariki dunia.

Taarifa za uhakika zinasema mpaka sasa mama huyo anao ujauzito wa miezi sita ambapo ameonelea ni vyema tu wakaweka wazi mahusiano yao na kuoana rasmi badala ya kuolewa na mdogo wa marehemu mume wake kama mila yao inavyotaka.

Mama Betty ameiambia mahakama ya kijiji chao kwamba ameanza mahusiano ya kimapenzi na mwanaye miaka mitatu iliyopita..."nimeanza mapenzi na mwanagu miaka mitatu iliyopita,nimepata shida sana kumsomesha mwanangu baada ya baba yake kufariki,hakuna mtu yoyote amenisaidia,sasa leo hii nafurahia matunda ya jasho langu nyie mnanishtaki...!!! tafadhali niacheni nifurahie matunda yangu."alifunguka mama Betty Mbereko.

Kwa upande wake mume mtoto bwana Farai amesema yupo tayari kumuoa mama yake na atalipa mahari yaliyosalia ambayo baba yake alikua anadaiwa kabla hajafariki ”ninajua baba yangu alifariki kabla hajamaliza kulipa mahari ya mama,kwa sasa najiandaa kupeleka malipo hayo ya mahari yaliyosalia,”alifunguka mume mtoto.

“ni vyema tukaweka wazi mahusiano yangu na mama,kwasababu nataka jamii ijue kwamba mimi ndio nimempa mimba mama yangu,vinginevyo najua watamyanyapaa sanaI

Msemaji wa kijiji hicho amesema kamwe hawawezi kukubali jambo hilo likubalike kwani itakua ni laana kwa kijiji chetu,.."kama ingekua ni zamani hawa watu wangepaswa kuuwawa,lakini kwa sasa hatuwezi kwasababu tunaogopa polisi na mahakama"alimalizia msemaji huyo wa kijiji.

0 comments:

Chapisha Maoni

 
Back to top!